• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

WAZEE MASASI WASHANGAZWA NA UBORA WA VIFAA TIBA NA MIUNDOMBINU MKOMAINDO, MTANDI NA MBONDE, WAMPONGEZA MHE. MWAMBE.

Posted on: July 15th, 2024

Baraza la Wazee Masasi limeshangazwa na ubora wa vifaa tiba na miundombinu inayopatikana katika vituo vya kutolea huduma za Afya mara baada ya kutembelea Hospitali ya Mkomaindo, Kituo cha Afya Mtandi na Kituo cha Afya Mbonde huku wakimpongeza Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mhe. Geoffrey Mwambe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mabadiliko hayo ya kihistoria katika vituo vya kutolea huduma za Afya Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara.  

Wamesema hayo Julai 15, 2024 katika ziara ya Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mhe, Geoffrey Mwambe akiambatana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mhe. Hashim Namtumba, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya Mhe. Ally Salvatory, Mganga Mkuu Dkt. Salum Gembe na wataalamu mbalimbali aliyoiandaa mahususi kwa ajili ya Baraza la Wazee Masasi kutembelea vituo vya kutolea huduma za Afya.

Wakizungumza Katika ziara hiyo, wamesema mabadiliko waliyoyashuhudia ni yakistoria na kuwaomba wananchi wafike katika vituo vya kutolea huduma za Afya kujionea wenyewe maboresho hayo makubwa ambayo hajayawahi kutokea kwa miaka mingi.  

“Kwakweli katika ziara hii, Nimefarijika sana kwa juhudi zake na usimamizi wake, Mhe. Geoffrey Mwambe, Wito wangu wananchi wengine waje Hospitali, ebu waje hospitali waone hospitali ilivyobora, ilivyokuwa na mambo ya kisasa na yakuridhisha na sisi Masasi tusiite masasi, napenda tuiite (New Masasi) kwa maana ya Masasi mpya, niwaombe wananchi wasiishie kusikia tu, waje wajionee wenyewe), Wamesema.  

Akizungumza katika ziara hiyo, Mhe Mwambe amesema mageuzi mbalimbali yamefanyika kuanzia majengo na vifaa tiba ili wananchi wa Masasi waweze kunufaika na huduma hizo.

“Mageuzi yamefanyika Mkomaindo na yanaendelea kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya, majengo tuliyojenga na huduma tunazotoa ziendane, Tubadilishe fikra ili kuleta imani kwa wananchi. Vituo vya afya Mtandi na Kituo cha Afya Mbonde tumevijenga  kwa ajili ya kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Mkomaindo na ili tubadili fikra ni muhimu Madaktari kutoa huduma kwa wakati, tuimarishe upande wa kujifungua, tuimarishe Upatikanaji wa dawa hospitali sambamba na huduma za mionzi”. Amesema

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mhe. Hashim Namtumba amesema kazi kubwa imefanyika katika maboresho hayo kilichobaki ni kubadili fikra na mitazamo kwa wananchi ambao bado wanamitazamo hasi za huduma za miaka ya zamani.

Mganga Mkuu, Dkt. Salum Gembe amesema ataendelea kusimamia masuala ya afya kwa ukamilifu na uadilifu ili utoaji wa huduma za Afya uendelee kuwa bora na kwamba kupitia Mkurugenzi wa Mji Masasi Ndg. Reuben Sixbert Jichabu wamejipanga kuhakikisha ubora na viwango  vya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi unaimarika na kwamba wanatarajia kufunga kamera za CCTV hospitali ya Mkomaindo ili kutazama mienendo ya utoaji wa huduma.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.