• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

WANANCHI MASASI KUNUFAIKA NA MRADI WA BARABARA MNIVATA-MASASI.

Posted on: June 22nd, 2023

Wananchi wa Halmashauri ya Mji Masasi wanakwenda kunufaika na ujenzi wa barabara ya Mnivata-Newala- Masasi yenye urefu wa kilometa 160 mara baada ya kukamilika kwa zoezi la Serikali kusaini mikataba miwili yenye gharama ya jumla ya Shilingi bilioni 234.512 inayokwenda kutatua changamoto ya usafiri na usafirishaji mkoani Mtwara.

Ujenzi wa barabara hiyo utaboresha mtandao wa barabara na madaraja kwa Ukanda wa kusini na hivyo kuboresha uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa June 21, 2023 na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe, Profesa Makame Mbarawa wakati akishuhudia utiaji saini wa mikataba hiyo katika hafla iliyofanyika viwanja vya Sabasaba wilayani Newala.

Profesa Mbarawa amesema ujenzi wa barabara hiyo utaboresha usafiri na usafirishaji wa malighafi za viwandani kama vile makaa ya mawe na saruji, mazao ya chakula na kilimo, bidhaa za biashara na mazao ya misitu, mifugo na uvuvi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

“Nachukua fursa hii kumpongeza sana Mhe, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja.., madhumuni ya ujenzi ujenzi wa barabara ya Mnivata-Newala- Masasi yenye urefu wa kilometa 160 ni kuwaondolea wananchi kero ya usafiri wa barabarani  na kuboresha mtandao wa barabara na madaraja ili kuongeza ufanisi katika sekta ya usafiri na usafirishaji ili kukuza uchumi wa wananchi, sasa mnakwenda kupata barabara bora na yenye viwango,” amesema Profesa Mbarawa

Mtendaji mkuu wa TANROADS, Eng. Mohamed Besta amesema mikataba hiyo ni baina ya Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) na kampuni ya China Wu Yi Co ltd itakayojenga barabara kutoka Mnivata-Mitesa (Km 100) kwa gharama ya Shilingi bilioni 141.964 na kampuni ya China Communications Construction Co. ltd itakayojenga sehemu ya pili kutoka Mitesa-Masasi (Km 60) pamoja na ujenzi wa daraja la Mwiti kwa jumla ya Shilingi bilioni 92.548.  

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Masasi mjini Mhe. Geoffrey Mwambe amesema ujenzi wa barabara hiyo unakwenda  kuwa mradi funganishi kuelekea mradi wa ujenzi wa standi kubwa ya kisasa ya mabasi ya Masasi.

“Tukae mkao wa kula uzinduzi wa mradi huu, ndio unapelekea rasmi kuanza mchakato wa mkandarasi wa ujenzi wa standi kubwa ya kisasa ya mabasi pale Masasi mjini, Masasi inakwenda kubadilika” amesema Mwambe

Hafla ya utiaji saini wa mikataba hiyo ilishuhudiwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Wakuu wa wilaya, Wenyeviti na wakurugenzi wa halmashauri, waheshimiwa madiwani, wabunge wa majimbo yote kutoka Mtwara, Wakuu wa idara na vitengo kutoka  halmashauri za Mtwara, wandarasi, wafanyakazi, watendaji wa Tanroads na wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.