• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO UNAENDA KWA KASI, BARAZA LA MADIWANI LAZUNGUMZA.

Posted on: November 8th, 2023

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Mji Masasi likiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Hashim Namtumba  limemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayowezesha ukuaji na ustawi wa wananchi wa Mji wa Masasi. 

Aidha limemshukuru Mhe, Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mhe. Geoffrey Mwambe kwa kupambana na  kuhakikisha miradi ya maendeleo inawafikia wananchi katika kata zote 14 za Halmashauri ya Mji Masasi.

Hayo yamebainishwa Novemba 8, 2023 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Robo ya Kwanza, 2023/2024  wa kupokea taarifa za kata uliofanyika katika Ukumbi wa Jengo la Utawala Halmashauri ya Mji Masasi.

Wajumbe wa kikao hicho waheshimiwa madiwani wa kata  wameelezwa kuwa miradi mbalimbali katika kipindi cha Robo ya kwanza imeendelea kutekelezwa kwa kasi ikiwemo ujenzi wa shule ya sekondari kata ya Jida, Ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo shule ya msingi Mkomaindo, Ujenzi wa bwalo, madarasa na vyoo shule ya sekondari Mwengemtapika, ujenzi wa nyumba ya walimu shule ya sekondari Temeke, ukamilishaji wa zahanati ya Napupa, ukamilishaji wa zahanati ya Matawale na Ujenzi wa Daraja Kata ya Marika.

Akizungumza Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Hashim Namtumba amesema utekelezaji wa miradi ya maendeleo unakuza Mji na kuimarisha maendeleo ya wananchi kiuchumi na kijamii.

" Taarifa ya kata ya Marika imewasilishwa na Diwani wa kata Mhe Asha Millanzi,  Kiupekee kuhusu daraja linalounganisha kati ya Nanyumbu na Masasi naomba tumpongeze sana Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mhe Geoffrey Mwambe kwa namna ambavyo amepambana kuhakikisha daraja lile linakuwepo, kwanza ni daraja kubwa sana, linatufungulia mlango wa mapato na  kwa umuhimu wake lile daraja kwa halmashauri yetu ni mlango wa uchumi kwasababu mazao yote" 

Naye, Diwani Kata ya Mwengemtapika Mhe. Mussa Millanzi ameshukuru kwa kupata fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata yake.

"Mhe Mwenyekiti napenda nishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya mama yetu  Mhe. Rais  Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea fedha kiasi cha Tsh milioni 320 Mwengemtapika sekondari kwa ajili ya ujenzi wa bwalo, madarasa na vyoo ikiwa ni kuhakikisha shule ile inaenda kutimiza lengo la Halmashauri ya Mji Masasi kuwa na shule ya kidato cha tano na sita". 

Aidha, Diwani kata ya Mkomaindo Mhe. Ally Salvatory amewashukuru wananchi kwa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa.

"Shule ya Msingi Mkomaindo kuna madarasa mawili yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi yameshafikia pamoja na hilo nishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea fedha kiasi cha Tsh milioni 208 za ujenzi wa maradasa 9 na matundu ya vyoo 16 na ujenzi upo kwenye hatua za ujenzi wa ukuta" Diwani kata ya Mkomaindo Mhe. 

Mkurugenzi wa Mji Masasi Ndg. Reuben Sixbert Jichabu amesema Malengo ya Halmashauri ni kukusanya mapato kwa wingi ili utekelezaji wa miradi ya maendeleo  uweze kutekelezeka kwa  ubora na wakati ili  wananchi huduma. 



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.