• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

“TEKELEZENI WAJIBU WENU KWA UFANISI” MHE. NAMTUMBA

Posted on: August 3rd, 2023


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mhe. Hashim Namtumba amewataka wakuu wa idara, vitengo na wataalamu kutekeleza wajibu wao kwa weledi na ufanisi ili kuchochea maendeleo ya halmashauri.

Amesema wataalamu wanatakiwa kuwa na uhalisia katika ukadiliaji wa fedha katika miradi ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Mhe. Namtumba amesema hayo agosti 3, 2023 katika mkutano wa Baraza la Madiwani Robo ya nne 2022/2023 uliofanyika katika ukumbi wa Jengo la Utawala.

“Mkurugenzi hoja hapa tuliyonayo ni kwamba hatujawahi kuona  fedha zinabaki kwenye mradi, kila mradi fedha hazitoshi hasa miradi inayotekelezwa na fedha kutoka serikali kuu” Mhe. Namtumba

Aidha amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kwenda kusimamia eneo la ukamilishaji wa miradi ili kuondoa changamoto iliyopo ya kutokamilisha miradi kwa fedha zilizotengwa kwenye mradi husika.

“Mkurugenzi hili ni baraza lake la kwanza ni vizuri sasa tukianza pamoja ili turuke pamoja, ukasimiamie eneo la ukamilishaji wa miradi ili tusiwe na miradi isiyokamilika” amesema.

Katika hatua nyingine amesema Baraza la Madiwani linamkaribisha Mkurugenzi mpya wa Halmashauri hiyo Bi. Erica Yegella kwa kuwa ni mara yake ya kwanza kushiriki katika mkutano wa Baraza la Madiwani.

Amesema waheshimiwa madiwani kwa pamoja wanamkaribisha mkurugenzi katika halmashauri hiyo na kwamba wapo tayari kwa dhati kushirikiana naye ili kuendeleza ustawi wa maendeleo ya halmashauri.

Mkutano wa baraza hilo ulihudhuriwa na waheshimiwa madiwani, wakuu wa idara na vitengo, wakuu wa taasisi mbalimbali, viongozi kutoka vyama mbalimbali,  viongozi kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa na wadau mbalimbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.