• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

RC MTWARA ASHANGAZWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI MASASI MJI, AZITAKA HALMASHAURI NYINGINE KUJA KUJIFUNZA MASASI

Posted on: June 21st, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Sawala ameshangazwa na utendaji kazi wa kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaofanywa na Mkurugenzi wa Mji Masasi Ndg. Reuben Sixbert Jichabu na watalaamu wake kwa kukamilisha miradi kwa wakati na ubora unaostahili huku akimuagiza Katibu Tawala Mkoa kuzileta Halmashauri zinazosuasua katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kuja kujifunza Halmashauri ya Mji Masasi.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema hayo leo 21 Juni, 2024  wakati wa ziara yake ya kuzungumza na watumishi sambamba na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Masasi hususani ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu nane ya vyoo katika shule ya sekondari Anna Abdallah.

“ Natambua uwepo wa Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Masasi, viongozi na watu wote, nashindwa niseme nini lakini jamani kuna watu wanatenda kazi, fedha imepokelewa tarehe 3/4/2024 leo jengo lipo hivi, nitoe shukurani na pongezi za dhati kwako Mhe,Mkuu wa Wilaya lakini Mkurugenzi na Timu yako yote ambayo inakusaidia katika uratibu, lakini wasimamizi kuanzia ngazi ya walimu, viongozi wa kata na wananchi wote kwa ujumla wake kwa kazi nzuri kama hii, RAS nikuombe katika wale ambao wanaosuasua katika miradi walete waje wajifunze Masasi, kazi ni nzuri”, Mhe Mkuu wa Mkoa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi, Ndg. Reuben Sixbert Jichabu amesema  mbali na Ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu nane ya vyoo katika Shule ya Sekondari Anna Abdallah, siku hiyohiyo tarehe 3/4/2024 fedha ilipokelewa Masasi Day kwaajili ya Ujenzi wa madarasa matatu na matundu nane ya vyoo sambamba na Nangose, darasa moja na matundu nane ya vyoo ambapo shule hizo mbili ujenzi wake umekamilika kwa kila kitu kinachosubiriwa ni wanafunzi kuingia darasani kusoma.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Anna Abdallah, Mwl, Zamoyoni Adam amesema shule hiyo ilipokea fedha kutoka Serikali kuu tarehe 3/4/2024 zaidi ya shilingi milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu nane ya vyoo.
Amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza tarehe 20/4/2024 na kwa mujibu wa mkataba  unatakiwa kukamilika 20/7/2024 lakini kutokana na kasi ya utekelezaji wa mradi mradi huo unatarajiwa kukamilika kabla au ifikapo 28/6/2024.


Aidha ametoa shukurani zake kwa Serikali katika kuhakikisha Mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji shuleni yanaboreshwa.


“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa Jumuiya ya Shule ya Secondari Anna Abdallah inatoa shukurani zake za dhati kwa Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya Shule ya Sekondari ili kutengeneza Mazingira mazuri ya ujifunzaji na ufundishaji mashuleni , Aidha jumuiya ya Shule ya sekondari inaendelea kutoa shukurani zake kwa Mhe. Geoffrey Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini na Mhe. Sospeter Nachunga, Diwani kata ya Napupa kwa ushirikiano wao mkubwa wanaoutoa katika utekelezaji wa mradi”. Mwl.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.