• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

RASMI ZAHANATI YA MATAWALE YAANZA KUTOA HUDUMA. MBUNGE MWAMBE AIFUNGUA.

Posted on: November 24th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mhe, Geoffrey Mwambe amefungua rasmi zahanati mpya ya kijiji cha Matawale Kata ya Matawale, Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara ikiwa ni ndani ya siku sita tu toka alipofungua zahanati mpya ya Machombe.

Hatua hiyo ameeleza kuwa ni mafanikio makubwa ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya  kuhakikisha wananchi wa Masasi Mji wanapata huduma bora za afya kwenye maeneo yao.

Ameeleza hayo, Novemba 24, 2023 wakati wa ufunguzi rasmi wa zahanati ya Matawale iliyopokea fedha kiasi cha Tsh milioni 150 kutoka Serikali kuu zilizotolewa kwa awamu tatu. 

Mhe. Mwambe amewataka watumishi katika zahati hiyo kuendelea kufanya kazi kwa kujitoa, ushirikiano, weledi na kuzingatia huduma bora sambamba na kuwaomba wananchi kuwapa ushirikiano watumishi hao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanajiunga na bima ya afya yenye gharama ya Tsh 30000 tu kwa mwaka kwa familia.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mhe. Hashim Namtumba amesema kuwa huo ni mwendelezo wa kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana na kuimarika na kwamba Halmashauri itakikisha inaendelea kuimarisha huduma za afya katika maeneo yote ya Mji Masasi.

Diwani wa kata ya Matawale, Mhe. Hamisi Mnela amesema ufunguzi wa kituo hicho ni alama kubwa kwa wananchi kwa kuwapunguzia umbali wa kutafuta huduma za afya huku akiwashukuru  Wananchi, Rais Dkt Samia na Mbunge Mwambe kwa kuhakikisha zahanati hiyo inakamilika na kufunguliwa.

Kaimu Mkurugenzi wa Mji Masasi, Ndg. Andrea Kalinga amewapongeza wananchi wa kijiji cha Matawale kwa kujitoa kwa nguvu kuhakikisha ujenzi huo unafanikiwa kwakuwa mchango wao ni mkubwa ukiwa na thamani ya fedha kiasi cha zaidi ya Tsh milioni tatu.

Mkuu wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Dkt. Salum Gembe amesema zahanati hiyo ni ya kisasa na bora na tayari watoa huduma za afya wameshaanza kutoa huduma katika zahanati hiyo.

Katibu Mwenezi wa chama cha mapinduzi  wilaya ya masasi Ndg. Twahili Mayola akimwakilisha Mwenyekiti wa CCM wilaya, amesema wananchi wanashuhudia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye maeneo ya Mji Masasi ikiwa ni pamoja na miradi elimu, barabara, maji na afya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.