• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

RAIS SAMIA AWAPA TABASAMU WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU

Posted on: August 13th, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt.  Samia Suluhu Hassan amewapa tabasamu watoto wenye mahitaji maalumu katika shule ya msingi Masasi iliyopo Halmashauri ya Mji Masasi Mkoani Mtwara kwa kutoa vifaa vya kuwasaidia na zawadi mbalimbali.

Akikabidhi Vifaa na Zawadi hizo agosti 13, 2023 kwa Uongozi wa shule ya Msingi Masasi, kwa niaba ya Rais, Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Mji Masasi Bi. Erica Yegella amesema Rais ameendelea kuwajali na kuwapa tabasamu watoto wenye mahitaji maalumu kwa kuhakikisha wanapata fursa bora ya elimu, mazingira bora, huduma bora za kijamii, upendo, amani na kila jema lenye kuchochea maendeleo ya watoto wenye mahitaji maalumu katika jamii.

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametoa zawadi nyingi na muhimu zitakazowasaidia wenye mahitaji maalumu  kwa muda mrefu.

“Nakabidhi zawadi mbalimbali kutoka kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan zikiwemo, White cane, Braille paper carton, Audible football/bell ball ,Universal braille kit, Braille slates with stylus, Perkins braille machines, Hand magnifies, Low vision stand, Albino special lotion tube, Albino special hat, Albino sunglasses, Puzzles, Rattles, Plastic building blocks, Push animal toys, Wallcharts animals, Wallchart alphabet, Wall chart numbers, Flash cards, Skipping ropes, Square wooden blocks, na Porcupine ball” Mkurugenzi

Aidha amesema binafsi anaunga mkono jitihada za Mhe. Rais Samia kwa kutoa bima za afya kwa watoto wote wenye mahitaji maalumu katika shule hiyo.

“ Mhe. Rais wetu ameshaleta vifaa vya kutosha hapa, na mimi binafsi namuunga mkono mheshimiwa Rais kwa kutoa bima za afya kwa watoto wote hawa, zoezi hili linaanza mara moja kwa watoto hawa kupigwa picha na kulipia bima zao, kwa sababu kuna magonjwa mbalimbali ni muhimu tulinde afya zao, bima hiyo nitaitoa mimi ”  Mkurugenzi Bi. Erica Yegella.

Amewakaribisha wananchi wa Masasi na wa maeneo mbalimbali kuendelea kutoa msaada wa vifaa na zawadi mbalimbali kwa watoto wenye mahitaji maalumu katika shule hiyo.

Katika hatua nyingine, Wadau mbalimbali na watumishi wameunga mkono juhudi hizo kwa kutoa zawadi mbalimbali ikiwemo chakula kama unga, mchele, sukari, maharage, mafuta, sabuni, vinywaji na zawadi mbalimbali.

Awali akisoma taarifa ya Shule hiyo, Mkuu wa shule  amesema shule ya Msingi Masasi ni shule ya Msingi Jumuishi iliyoanzishwa mwaka 1954 ikiwa na jumla ya wanafunzi 626 ambapo wavulana ni 318 na wasichana 308.

Amesema kati yao wenye mahitaji maalumu ni 65 ambapo wavulana ni 35 na wasichana 30 wakiwa katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza ni wasioona wakiwa 30, wenye ulemavu wa ngozi ( albinism) 26, na walemavu wa viungo 8.

Amesema zawadi hizo zitawasaidia sana katika kuboresha afya zao na maendeleo yao kielimu kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.