• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Masasi akabidhi mabati 20 kwa Shule ya Msingi Mbonde

Posted on: May 21st, 2020

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano – Masasi Mji

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mheshimiwa Selemani Mzee amekabidhi mabati ishirini (20) yenye thamani ya shilingi 500,000/= kwa Serikali ya Kijiji na Kamati ya Shule ya Msingi Mbonde ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Gaspar Byakanwa aliyoitoa mnamo tarehe 30/01/2020 alipotembelea Shuleni hapo.

Makabidhiano hayo yamefanyikia Shule ya Msingi Mbonde iliyopo Kata ya Mwenge Mtapika, Halmashauri ya Mji Masasi. Wananchi wa Kijiji cha Mbonde waliibua mradi wa ujenzi wa matundu kumi (10) ya vyoo ikiwa ni sehemu ya kuitikia Kampeni ya Shule ni choo iliyoasisiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mwishoni mwa mwaka jana 2019.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mabati hayo, Mheshimiwa Mzee amewaasa Wananchi wa Mbonde kumtia moyo Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwa kumuonesha ya kwamba mchango wake huo ambao ameutoa kwenye Shule hiyo unatumika ipasavyo na kwa wakati ili kuwasitiri Wanafunzi wa Shule hiyo ya Msingi.

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya alitumia hadhara hiyo kuiagiza Halmashauri ya Mji Masasi ikamilishe miradi iliyoibuliwa kwenye Kampeni ya Shule ni choo ili Shule zitakapofunguliwa baada ya kuisha kwa janga la ugonjwa wa Covid-19, Wanafunzi wa Shule husika wakute miundo mbinu ya vyoo hivyo imekamilika.

Sambamba na hilo, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ameagiza uongozi wa ngazi zote unaozisimamia Shule za Msingi na Sekondari Wilayani humo kuhakikisha Shule zinafanyiwa usafi wa mazingira ili zitakapofunguliwa Wanafunzi waanze masomo, na siyo kutumia wiki nzima au zaidi kuyafanyia usafi mazingira ya Shule hizo. Aidha, amesisitiza kuimarishwa kwa ulinzi kwenye mazingira ya Shule zote ili kusitokee uharibifu wa mali na miundombinu ya Shule katika kipindi hiki cha likizo.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji cha Mbonde, Kaimu Mwenyekiti wa kijiji hicho ndugu Mussa Zuberi Millanzi, alimshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kwa kuguswa na mradi huo wa matundu kumi (10) ya vyoo vya wanafunzi, na kwamba mabati hayo ishirini (20) yatatosha kuezekea jengo hilo la vyoo vya wanafunzi kulingana na bajeti. Aliahidi ya kwamba mabati hayo yaliyotolewa yatatumika kama ilivyokusudiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.