• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MKUU WA MKOA MTWARA ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA HALMASHAURI YA MJI MASASI

Posted on: November 29th, 2021

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano  – Masasi Mji

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Brigedia Jenerali Marco Gaguti ameipongeza Halmashauri ya Mji Masasi kutokana na kasi nzuri ya ujenzi wa vyumba vya madarasa unaoendelea katika Halmashauri hiyo. 

Mhe. Brigedia Jenerali Gaguti ametoa pongezi hizo leo tarehe 29/11/2021 baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa ujenzi na kisha kutembelea Shule zinazotekeleza mradi huo wa ujenzi wa vyumba vya madarasa ambazo ni Shule za Sekondari Nangaya, Chanikanguo, Mtandi, Mtapika, Marika, na kisha Kata ya Mtandi ambako kunajengwa Kituo cha Afya. Ujenzi huo wa vyumba vya madarasa upo katika hatua za ukamilishaji wakati mradi wa Kituo cha Afya upo katika hatua ya kujenga boma.

Mhe. Mkuu wa Mkoa, amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi Ndugu Elias Ntiruhungwa kwa kusimamia vizuri ujenzi huo akisema kwamba Mkurugenzi huyo ni mfano wa kuigwa.

Halmashauri ya Mji Masasi ilipokea jumla ya shilingi milioni 820 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 37 vya madarasa pamoja na ujenzi wa Bweni moja la Wanafunzi wenye mahitaji maalumu wanaosoma Shule ya Msingi Masasi.

Aidha, Halmashauri ya Mji Masasi ilipokea mgao wa fedha iliyotokana na tozo za miamala ya simu kiasi cha Shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha kimkakati Kata ya Mtandi. 

Katika hatua nyingine, Mhe. Mkuu wa Mkoa alipata wasaa wa kuongea na Wananchi wa Kata za Chanikanguo na Mwenge Mtapika ambapo amewasisitiza kulinda amani na usalama katika maeneo yao, kuwekeza katika Elimu ya watoto wao, na kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi inayoendeshwa kwenye maeneo yao kwa kujitolea. 

Katika ziara hiyo, Mhe. Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa Mhe. Abdallah Mohamed Malela pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.