• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MASASI MJI YAPANDA KWA KASI UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE

Posted on: February 25th, 2025

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Masasi Bi. Renalda Mbowe amesema hali ya utekelezaji wa afua za lishe kwa jamii inazidi kuimarika na kuboreshwa mara baada ya Halmashauri ya Mji Masasi kupanda  kwa kasi kutoka nafasi ya nane kimkoa kwa mwaka wa fedha  2022/2023 hadi nafasi ya tatu kimkoa kwa mwaka 2023/2024 katika usimamizi wa utekelezaji wa afua za lishe.

Amesema hayo mara baada ya kukabidhiwa cheti cha pongezi kilichotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Sawala na kukabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Mji na Mratibu wa Lishe Masasi Mji Bi. Happiness Mlamka ambapo Halmashauri ya Mji Masasi imepata cheti cha pongezi kwa kuibuka mshindi wa tatu katika usimamizi wa utekelezaji wa afua za lishe kwa mwaka wa fedha 2023/2024. 

Aidha amewataka watalaam kuendelea kuimarisha usimamizi wa afua za lishe kwa kutoa elimu kwa jamii kuhusu lishe bora na athari zitokanazo na lishe duni ikiwemo udumavu, magonjwa yasiyoambukiza na kuhamasisha jamii kuhusu upatikanaji wa chakula shuleni ili Halmashauri iendelee kupanda kwa kasi kimkoa na kitaifa kwa ujumla. 

Hayo yamejiri leo Februari  25, 2025 katika kikao cha Kamati ya Lishe Robo ya Pili, 2024/2025 kilichofanyika katika Ukumbi wa Jengo la Utawala ambapo watalaamu wameeleza taarifa za lishe kwa upande wa elimu ya awali na msingi, elimu sekondari, kilimo, mifugo na uvuvi, Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe. 

Kikao hicho kimejadili kwa kina hali ya lishe shule za msingi na sekondari, hali ya utapiamlo, matibabu ya utapiamlo mkali, unyonyeshaji maziwa ya mama ndani ya lisaa la kwanza, Watoto waliozaliwa na uzito pungufu, Watoto wanaopata chakula shuleni na ukaguzi na uhamasishaji wa matumizi ya vyakula vilivyoongezewa virutubishi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.