• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

“KUKUSANYA MAPATO NDIO KIPAUMBELE CHANGU” MKURUGENZI YEGELLA.

Posted on: August 3rd, 2023

Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Masasi, Bi. Erica Yegella amesema kipaumbele cha kwanza atakachokisimamia katika mwaka wa fedha 2023/2024 ni ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ili utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia mapato ya ndani uweze kutekelezeka na kukamilika kwa wakati.

Amesema hayo Agosti 3, 2023 ikiwa ni mara yake ya kwanza kuhudhuria na kushiriki mkutano  wa Baraza la Madiwani Robo ya nne 2022/2023 uliofanyika katika ukumbi wa Jengo la Utawala.

Amewaomba waheshimiwa madiwani kutoa ushirikiano katika maeneo yao hususani katika ukusanyaji wa mapato kwa kuwa wao ni wenyeji wa vipenyo vya mapato.

“Na niwe wazi kwenu waheshimiwa madiwani mimi natafuta mapato ili nikatekeleze miradi hususani miradi ya mapato ya ndani, na ukweli usiopingika sitadandia mradi, nitatekeleza yale mliyoagiza kwenye bajeti” Mkurugenzi.

Katika Baraza hilo, Bi. Yegella amesema ataendelea kusimamia kwa ukamilifu utendaji kazi wa watumishi ili kila mmoja awajibike kwa ukamilifu na weledi.

“Niwashukuru sana sijawahi kuona Baraza zuri la Madiwani kama hili, baraza pendwa na linasema ukweli, na mimi kama mtendaji inanipasa nikawajibike, nimeyasikia yote na nimeyapokea,”

Amesema hatasita kumchukulia hatua mtumishi yeyote atakayekwenda kinyume na taratibu, sheria, kanuni na miongozo ya utendaji kazi ili Halmashauri itekeleze miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa wananchi.

“Mimi mheshimiwa Mwenyekiti sitakuwa na maneno mengi, ninatabasamu sana ila kumunyoosha mtu sioni shida, mimi ninafuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo” Bi Erica.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA MJI MASASI 2025-2030

    December 03, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAMPONGEZA MKURUGENZI JICHABU UNUNUZI WA RTK NA KUPELEKA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI KWENYE MIRADI YOTE ILIYOTENGEWA FEDHA 2025/2026

    December 02, 2025
  • MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA MJI MASASI WAFANYIKA

    December 02, 2025
  • MPYA: HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA MUDA WOTE HOSPITALI YA MKOMAINDO

    November 28, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.