• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

KAMATI YA MTAKUWWA YATAKIWA KUONGEZA KASI UTOAJI ELIMU YA UKATILI

Posted on: August 7th, 2023

Mwenyekiti wa Kamati ya Mpango wa kudhibiti  ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) Halmashauri ya Mji Masasi ambaye pia  ni Mkurugenzi wa Mji Masasi  Bi. Erica Yegella amesema ni muhimu kuangalia namna bora ya utoaji wa elimu dhidi ya ukatili wa wanawake na Watoto ili kumaliza changamoto ya ukatili katika jamii.

Ametoa wito huo Agosti 7,2023 katika kikao cha kamati ya MTAKUWWA robo ya nne 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa jengo la Utawala Halmashauri ya Mji.

Amesema Mpango wa Taifa wa kudhibiti ukatili dhidi ya wanawake na Watoto (MTAKUWWA) unatekelezwa katika ngazi ya Taifa, Mkoa na Serikali za Mitaa kupitia watalaamu mbalimbali na wanajamii wote.

Amesema elimu ya ukatili katika jamii inatolewa lakini ni vyema sasa kutazama namna na mbiu za ufundishaji, uelekezaji na namna ya kufikisha na kupokea ujumbe wa ukatili ili jamii na wahanga wawe wazi kueleza changamoto wanazokumbana nazo.

“Mimi nafikiri tubadilishe namna ya ufundishaji na tukiwatumia viongozi wetu wa dini, vijana na hata kuunda klabu ya Mtakuwwa katika shule zetu za msingi, klabu inayoweza kujumuisha wanafunzi katika kila darasa, tutapiga hatua kubwa sana katika kupunguza ukatili” Mwenyekiti.

Amesema kasi ya utoaji elimu inapaswa kuongezeka  ili jamii iwe na muamuko wa ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto

“lakini pia ni muhimu tupunguze ukatili na matukio yasiyopendezeka machomi kwa binadamu  kwasababu wewe kama binadamu na elimu inakuwaje unaendeleza ukatili? mimi nataka tupunguze ukatili ili tufanye Masasi iwe sehemu ya kurelax, mtu akija hapa anaishi vizuri, anakula vizuri , analala vizuri, anatembea anasikia raha, Barabara safi kila kitu kinakuwa safi” Mwenyekiti.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Masasi, Dkt. Salum Gembe amesema katika kuhakikisha Mpango wa Taifa wa kudhibiti ukatili dhidi ya wanawake na Watoto (MTAKUWWA) unatekelezwa katika ngazi ya Halmashauri  elimu ya ukatili wa kijinsia   itazidi kutolewa kwa kushirikiana na dawati la jinsia kutoka Polisi, asasi za kiraia na jamii kwa ujumla.

Kikao cha MTAKUWWA robo ya Nne 2022/2023 kilihudhuliwa na wajumbe mbalimbali na wadau kutoka kwa wawakilishi wa makundi yote muhimu katika jamii ikijumuisha viongozi wa dini, wawakilishi kutoka makundi maalumu, mwakilishi wa Watoto na wanafunzi, watalaamu wa afya, kamati ya ulinzi na usalama, dawati la jinsia kutoka polisi, na maafisa elimu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.