• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

KAMATI YA LISHE MASASI MJI YAPONGEZWA KWA KUTEKELEZA MPANGO WA UPATIKANAJI CHAKULA SHULENI

Posted on: July 26th, 2023

Kamati ya Lishe Halmashauri ya Mji Masasi imepongezwa kwa kuwezesha utekelezaji wa mpango wa upatikanaji wa chakula shuleni kwa asilimia 100  huku ikitakiwa kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa wazazi  na jamii juu ya umuhimu wa wazazi kuchangia upatikanaji wa chakula ili kuongeza kiwango cha upatikanaji wa lishe bora shuleni.

Pongezi hizo zimetolewa Julai 26, 2023 na Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe Ndg, Andrea Kalinga akimwakilisha Mwenyekiti wa Kamati ya lishe (Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji), wakati wa kikao cha kamati ya Lishe Robo ya Nne 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa Jengo la Utawala Masasi Mji.

Amesema pamoja na hilo elimu kupitia vikao na wazazi, walezi na jamii inatakiwa kuendelea kutiliwa mkazo ili wazazi wote watambue kwa kina  umuhimu wa upatikanaji wa chakula shuleni kwa wanafunzi wote sambamba na kuendeleza bustani za mbogamboga, miti ya matunda na kupanda mimea jamii ya kunde katika maeneo ya shule ili kuchangia upatikanaji wa lishe bora shuleni.

“lakini pia tukaangalie namna ya kufanya hasa kuongea  na wadau kama Sanku kwakuwa anatoa mashine za kuchanganya virutubisho kwenye unga wa kusaga, virutubisho, na mifuko ya kufungasha, basi tuombe hata mashine ili waweze kuongeza virutubisho hivyo kwa ajili ya vyakula vya wanafunzi ”  Ndg. Kalinga

Awali, akieleza kuhusu utekelezaji wa afua za lishe kwa shule za msingi na sekondari, Mratibu wa Lishe Halmashauri ya Mji Masasi, Bi. Happiness Mlamka amesema jumla ya shule zinazotekeleza mpango wa upatikanaji wa chakula shuleni ni 56 ambazo ni sawa na asilimia 100 kwa kuwa ndio jumla ya shule za msingi na sekondari zinazopatikana katika halmashauri hiyo.

Amesema suala la lishe ni suala mtambuka hivyo ni muhimu ushiriki wa kila mmoja katika taasisi na jamii kujitoa kwa dhati ili kutimiza malengo ya upatikanaji wa lishe bora kwa wanafunzi wote kwani asilimia 41.66 ndio  waliopata chakula  kwa mwaka 2022/2023.

“Suala la lishe jamani ni suala mtambuka, wote hapa tunapaswa kujitoa kwa dhati kwa kuweka  shughuli za kufanya (activity) katika idara zetu, kuanzia maendeleo ya Jamii, Elimu, Kilimo na uvuvi lakini kama fedha imetengwa kwa ajili ya  lengo (objective Y) itumike kukamilisha lengo Y pekee na sio kuhamisha hamisha fungu, tuzidi kuzingatia hili ili tuzidi kupata alama”   Bi. Happiness

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.