• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI LAZINDULIWA HALMASHAURI YA MJI MASASI.

Posted on: November 9th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi Mhe. Hashim Namtumba amezindua rasmi jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi na kukabidhi mwongozo wa uendeshaji wa jukwaa hilo kwa ngazi ya Halmashauri.

Amezindua na kukabidhi mwongozo wa uendeshwaji wa jukwaa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa hilo ngazi ya Halmashauri Bi. Mariam Ngole, Novemba 9, 2023 katika ukumbi wa Jengo la Utawala.

Mhe. Namtumba, amesema malengo ya uanzishwaji wa jukwaa hilo ni utekelezaji wa malengo 17 ya dunia kati yake ni yale  yanayohimiza ushiriki wa wanawake kwenye shughuli za maendeleo na za kijamii na ushirikishwaji wa 50/50.

Amesema malengo hayo yanasimamiwa vyema na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan na kwamba jukwaa hilo litakuwa endelevu na litapata uungwaji mkono kutoka halmashauri.

"Jukwaa hili tunaamini litakuwa endelevu na litasimama vizuri sana, sisi kama halmashauri hatutatenda haki kama tutawaacha muende pekee yenu, ni lazima sisi tushiriki kwa nafasi yetu kama halmashauri, leo tumezindua na kutoa mwongozo wa uendeshaji wa jukwaa hili" Mhe. Namtumba.

Amesema lengo ni kuhakikisha wanawake  wanapata haki sawa katika ngazi za uongozi, utawala na uchumi.

Katibu wa Umoja wa wanawake wilaya ya Masasi, Martina Katyale amesema pamoja na mambo mengine lengo la jukwaa hilo ni kuwaunganisha wanawake ambao wapo hali ya chini na kuwainua kiuchumi ili waweze kulingana na wanawake wote kiuchumi.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake kiuchumi Halmashauri ya Mji Masasi, Mariam Ngole amesema wanawake wasisite kumfikia kwaajili ya utekelezaji, ukuaji na ustawi wa jukwaa hilo na kwamba atashirikiana na kila mwanamke kwa kutoa elimu, maoni na mawazo ili wanawake wote wakuze uchumi wao.

Jukwaa hilo katika ngazi ya halmashauri linaongozwa na Mwenyekiti wake, Mariam Ngole, Makamu mwenyekiti Mwajuma Kamundi, katibu wake Bi. Leah Amuli, Katibu msaidizi Agnes Zawadi na Mweka hazina, Mwajuma Dadi na wajumbe. 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.