• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

"TUTAENDELEA KUIMARISHA ZAIDI USHIRIKIANO WETU NA ENZKREIS" NDG. JICHABU

Posted on: November 24th, 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi Ndg. Reuben Sixbert Jichabu amesema ziara  ya ugeni wa marafiki wa Masasi kutoka wilaya ya Enzkreis ya nchini Ujerumani  ni ishara ya kuendelea kuimarisha uhusiano huo wa muda mrefu uliopo kati ya Masasi na Enzkreis katika nyanja mbalimbali ikiwemo Afya, Mazingira hususani  kuongeza ushirikiano katika suala la udhibiti taka , elimu, ujuzi na kubadilishana uzoefu kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Masasi.

Amebainisha hayo  katika hafla ya kuwakaribisha wageni hao akiwemo Bi. Angela Gewiese mratibu wa miradi ya ushirikiano Enzkreis na Masasi, Daktari bingwa Dr. Nils Herter kutoka hospitali ya Enzkreis ujerumani, Ulrich Klotz, Afisa Muhifadhi Misitu kutoka ofisi ya misitu ya Enzkreis, na Daktari bingwa wa mifupa Dr. Lunemo Sakafu kutoka Mbeya Refferal Hospital katika (welcome dinner) iliyofanyika katika mgahawa uliopo kituo cha elimu ya mazingira Novemba 24, 2025.

Katika hafla hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi, Ndg. Jichabu alisema,

“Ziara yenu ni ishara ya kuendelea kuimarisha uhusiano huu wa muda mrefu uliopo kati ya Masasi na Enzkreis katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Afya, Mazingira, elimu, ujuzi na kubadilishana uzoefu, lakini pia ni matarajio yetu kwamba tutaongeza ushirikiano zaidi katika suala la udhibiti wa taka, ni suala muhimu sana nadhani mtapata muda wa kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo dampo letu, mtajionea wenyewe lakini pia nashukuru ujio wa madaktari bingwa wa mifupa kwa ajili ya kutoa huduma ya matibabu hospitali ya Mkomaindo na kubadilishana uzoefu na madaktari wa Masasi”

Wilaya ya Enzkreis ya Nchini Ujerumani, Halmashauri ya Mji Masasi, Halmashauri ya Wilaya Masasi, TAREA na TFS wanaendelea kushirikiana kwa pamoja kupitia miradi mbalimbali kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Masasi.

Kwa pamoja wanatekeleza mradi wa NAKOPA  kwa mwaka wa fedha 2025/2026 mpaka mwisho wa mwaka 2027.

Mradi huo wenye jina la Shule za kijani, upandaji miti, uvunaji wa maji na elimu ya Mazingira kwa ajili ya Maendeleo endelevu Masasi, Unalenga kuboresha mazingira, kuongeza upatikanaji wa maji mashuleni, elimu juu ya nishati mbadala na nishati safi ya kupikia na kuimarisha elimu ya uhifadhi mazingira kwa wanafunzi na jamii ya Masasi kwa ujumla.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • "TUTAENDELEA KUIMARISHA ZAIDI USHIRIKIANO WETU NA ENZKREIS" NDG. JICHABU

    November 24, 2025
  • RIPOTI ZA MIRADI

    November 18, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI ATANGAZA MATOKEO YA NAFASI YA UBUNGE JIMBO LA MASASI MJINI.

    October 31, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI NA MAKARANI WAONGOZAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA UCHAGUZI MKUU 2025

    October 21, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.