• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

Posted on: April 7th, 2025

Jumla ya Tsh Milioni 148 zimetolewa kwa vikundi 30 katika Hafla ya Utoaji wa Mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu iliyotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani Halmashauri ya Mji Masasi kwa awamu ya pili mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuridhia na kurejesha mikopo hiyo ili kuwasaidia wananchi kiuchumi.

Akizungumza mbele ya mgeni rasmi, April 7, 2025 katika utoaji wa mikopo hiyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi Ndg. Reuben Sixbert Jichabu amesema zaidi ya Tsh milioni 545 zimetolewa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwa vikundi 105 ambapo awamu ya kwanza vilipokea vikundi 75 na hivi sasa vikundi 30. 

Amesema mafanikio hayo ya utekelezaji wa maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan yamefikiwa  na kuandika historia hiyo kutokana na usimamizi mzuri kutoka kwa viongozi mbalimbali, Baraza la Madiwani chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Hashim Namtumba na Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini Mhe. Geoffrey Mwambe hususani kuhakikisha wananchi wanaimarika kiuchumi. 

Akikabidhi hundi ya Tsh milioni 148 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Rachel Kassanda amesema kuwa lengo la kutoa fedha hizo hadharani ni kuwafanya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu waone umuhimu wa kuanzisha vikundi ili wapate fursa za kupata mikopo hiyo ili wastawi kiuchumi na kijamii.

 “Imani yangu kubwa tutakapo kusanya fedha zingine tena tutaleta hundi kwa ajili ya vijana wengine wapya,wanawake pamoja na watu wenye ulemavu, ni muhimu tufanye kazi kwa kuwa Serikali imeendelea kutengeneza mazingira bora ya kiuchumi kwa wananchi” amesema. 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi Mhe. Hashim Namtumba amesema waheshimiwa madiwani wamefanya kazi muhimu kuhakikisha mikopo hiyo inatolewa ili kuwezesha ustawi wa wananchi na kwamba hakuna kikundi kilichopata kwa upendeleo na hivyo vikundi vyote vikawe mabalozi wa kusema mazuri ya Serikali na Halmashauri. 

Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Bi. Neema Joseph amesema  katika vikundi 30, wanawake wamepokea Tsh 77,800,000 kwa vikundi 17, Vijana Tsh 68,000,000 kwa vikundi 11 na watu wenye ulemavu Tsh milioni 2,200,000 kwa vikundi viwili. 

 

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • .STANDI YA MAEGESHO YALETA FURSA KWA WANANCHI MASASI.

    March 22, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.