Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda (MB), amemkabidhi Hundi ya Shilingi Milioni Mbili na Laki Tano pamoja na cheti cha pongezi Mwalimu Haji Mohamedi Ligalawa wa Shule ya Msingi Mtandi iliyopo Halmashauri ya Mji Masasi kwa kuibuka mshindi wa tatu kati ya washiriki 148 katika Shindano la Stadi za Ufundishaji wa Masomo ya Sayansi kwa shule za Msingi.
Zawadi hiyo imetolewa Juni 14, 2025, katika Ukumbi wa Maktaba Mpya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Waheshimiwa Wabunge, na viongozi wa Taasisi mbalimbali.
Akiongea baada ya Hafla hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mji Masasi, Kaimu Afisa Elimu ya Awali na Msingi Halmashauri ya Mji Masasi Mwl. Joseph Amlima, ameipongeza Taasisi ya Elimu Tanzania kwa Kuandaa Mashindano hayo ambayo huwafanya Walimu kuwa bora zaidi.
Aidha amempongeza Mwl. Haji Ligalawa kwa ushindi huo mkubwa kwa kubainisha kuwa ameiheshimisha Halmashauri ya Mji Masasi na Mkoa wa Mtwara kwa Ujumla wake huku akitoa wito kwa Walimu wote wa Mji Masasi kuendelea kujitokeza kwenye Mashindano hayo ili waweze kuonesha umahiri wao katika ufundishaji na ubunifu unaozingatia Mtaala Mpya wa Elimu.
Shindano hilo huandaliwa kila mwaka na Taasisi ya Elimu Tanzania kwa ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji kwa Shule za Awali na Msingi BOOST.
Kwenye picha upande wa kulia aliyevaa miwani ni Kaimu Afisa Elimu ya Awali na Msingi Halmshauri ya Mji Masasi Mwl. Joseph Amlima, Waziri wa elimu (katikati) na mshindi mwalimu Haji.
MASASI TOWN COUNCIL
Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI
Simu Ya Mezani: +255 23 2510685
Simu ya Kiganjani:
Barua pepe: info@masasitc.go.tz
Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.