Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Rachel Kassanda leo Juni 15, 2025 ameongoza maelfu ya wananchi kutoka Tanzania Bara na Visiwani katika mazoezi ya mbio za pole pole katika bonanza la “Umoja Jogging Club, Samia Bonanza Masasi” zilizoambatana na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kuona wagonjwa Hospitali ya Mkomaindo na kutamatika katika Uwanja wa Sabasaba kata ya Mkuti Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara.
Akizungumza mara baada ya kutembelea wagonjwa asubuhi na Jioni ya leo, Mhe. Kassanda, amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia “Samia Bonanza Masasi” ameleta tabasamu kubwa kwa kuwapa faraja wagonjwa kwa kutoa zawadi mbalimbali ambazo zitawasaidia kwa kiasi kikubwa katika matumizi yao.
Nao, baadhi ya wanawake waliojifungua katika Hospitali ya Mkomaindo wametoa shukurani zao za dhati kwa kupewa zawadi hizo na kusema kwamba huduma mbalimbali wanazopatiwa Hospitalini hapo ni bora, kisasa, zenye weledi na viwango.
Bonanza hilo limeambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo kuchangia damu salama, Kupima VVU, kupima malaria bure, elimu ya ujasiriamali, biashara na uwekezaji, elimu ya utalii na kuona wagonjwa katika Hospitali ya Mkomaindo.
MASASI TOWN COUNCIL
Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI
Simu Ya Mezani: +255 23 2510685
Simu ya Kiganjani:
Barua pepe: info@masasitc.go.tz
Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.