• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

Posted on: April 6th, 2025

Wataalamu wa Afya kutoka Halmashauri ya Mji Masasi wakiongozwa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Masasi Dkt. Salum Gembe wametoa elimu ya tahadhari juu ya ugonjwa wa Mpox katika Kanisa la Anglikana lililopo Mtaa wa Wapiwapi.

Ikumbukwe kuwa, Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama March 15, 2025 aliwataka wataalamu wa afya Nchini kuendelea kutoa elimu kwa Watanzania ya kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Mpox.

Akizungumza wakati wa kutoa elimu ya tahadhari  juu ya ugonjwa huo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Masasi Dkt. Salum Gembe amesema kuwa ni vyema wakazi wa Masasi kuchukua tahadhari mapema ili kujikinga na ugonjwa huo kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Aidha Dkt. Gembe amewataka wananchi kutoa taarifa haraka wanapoona kuna mtu ana dalili za ugonjwa huo ili wataalamu wamfanyie vipimo na kudhibiti hatari zaidi kwa wengine.

Naye, Afisa Afya wa Halmashauri ya Mji Masasi, Benjamin Shilinde akitoa elimu juu ya ugonjwa huo amesema kuwa dalili za ugonjwa wa Mpox ni kama vile kutoka vipele vikubwa usoni na sehemu zote za mwili na kuvimba mitoki ya mwili.

Pia ameweka wazi jinsi ugonjwa wa Mpox unavyoweza kuambukizwa kwa njia kama vile kugusa majimaji ya mwili wa mtu mwenye maambukizi ya Mpox, kugusana na mtu mwenye dalili za Mpox, kugusa vitu vilivyotumiwa na mtu mwenye maambukizi ya Mpox na kula au kugusa mizoga au wanyama pori walioambukizwa mfano nyani, sokwe, tumbili au swala wa msituni.

Aidha alieleza namna ya kujikinga na ugonjwa wa Mpox kwa njia kama kuepuka kusogeleana karibu na mtu mwenye dalili za Mpox, epuka kugusa vyombo, matandiko, nguo au godoro la mtu mwenye ugonjwa wa Mpox, epuka kugusa majimaji ya mwili wa mtu mwenye Mpox, epuka kusalimiana kwa kukumbatiana, kubusiana au kushikana mikono na mtu mwenye maambukizi ya Mpox, nawa mikono yako mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni au tumia vitakasa mikono, vaa barakoa ikiwa unaongea na mtu mwenye dalili za Mpox, epuka kula au kugusa mizoga au wanyama pori wenye maambukizi, ziba mdomo kwa kiwiko unapokohoa au kupiga chafya, safisha na takasa sehemu zote na vitu ambavyo vinaguswa mara kwa mara, pia epuka kugusana na mtu mwenye dalili za Mpox.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.