• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

“TUMEPATA MAPOKEZI MAZURI ” DKT HILDE

Posted on: July 23rd, 2023


Makamu wa Rais Halmashauri ya Enzkreis ya Nchini Ujerumani, Dkt. Hilde Neidhardt amesema wamefurahishwa na mapokezi waliyoyapata Masasi mkoani Mtwara hususani kupelekwa kufanya utalii katika mto Ruvuma na Pori la Akiba Lukwika Lumesule linalosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania.

Amesema hatua za halmashauri za Masasi Mji na Wilaya kuwapeleka kujionea utalii inazidi kuimarisha ushirikiano na mahusiano baina ya Enzkreis na Masasi.

Amebainisha hayo July 23, 2023 mara baada ya kutembelea na kujionea vivutio mbalimbali vya utalii katika pori la akiba Lukwika Lumesule ikiwemo wanyama, miamba ndani ya mto Ruvuma na pango la Habiba lenye historia ya kipekee.

Naye, Mratibu wa ushirikiano huo kutoka Enzkreis, Bi. Angela Gewiese amesema ushirikiano kati yaEnzkreis na Masasi ulianza miaka 12 iliyopita na umezidi kuimarika zaidi.

“mimi ndiye mratibu wa ushirikiano kati ya Enzkreis, mji wa Masasi, na halmashauri ya wilaya ya Masasi. Ushirikiano huu umekuwepo kwa miaka 12, na nimefurahishwa sana kutembelea eneo la hifadhi ya wanyama ya Lumesule kwa sababu wakati wa ziara yetu ya kwanza mwaka 2013, eneo hili lilikuwa halina kitu chochote. Kwa hivyo, tunavutiwa sana na maendeleo ya hifadhi hii ya wanyama na kushuhudia jinsi mambo yalivyobadilika kwa wakati huu, sasa tuna askari wa uhifadhi na jengo la maonyesho ambapo watu wanaweza kuja kutembelea. Ni jambo zuri sana kuona jinsi utalii unavyokua hapa”. Bi Angela.

Ujumbe kutoka Halmashauri ya Enzkreis nchini Ujerumani umeongozwa na Makamu wa Rais wa Enzkreis, Dkt. Hilde Neidhardt, mratibu wa ushirikiano huo, Bi. Angela Gewiese, Frank Stephan, Dkt. Jannis Hoek, Melissa Gewiese na Dkt. Till Neugebauer.

Ushirikiano baina ya Enzkreis na Masasi umezidi kuimarisha uboreshaji wa miundombinu ya umeme hususani matumizi ya nishati ya jua kwa kutumia sola yanayolenga kuboresha mazingira na miradi mbalimbali inayotekelezwa kutokana na ushirikiano huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.