• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MRADI WA KITUO CHA ELIMU YA MAZINGIRA WATAMBULISHWA RASMI KWA WANANCHI.

Posted on: August 24th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Masasi akiwakilishwa na Afisa Tarafa Halmashauri ya Mji Masasi, Ndg. Fikiri Lukanga ametambulisha rasmi mradi wa kituo cha Elimu ya Mazingira kwa wananchi uliogharimu zaidi ya Tsh milioni 242 huku akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha Mazingira ya wawekezaji na wafadhili yanaboreshwa, Serikali ya Ujerumani Landratsamt Enzkreis, Wizara ya Maendeleo ya Ushirikiano wa Kiuchumi Ujerumani, Taasisi ya Engagement Global ya Ujerumani, Taasisi ya Service Agency Ujerumani pamoja na Taasisi ya TAREA kwa kuwezesha kituo hicho.  

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mhe. Hamisi Nikwanya kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri amesema ushirikishwaji wa wadau mbalimbali kama Wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo vya kati, makundi maalumu, akina mama wajasiriamali na wananchi kwa ujumla katika utoaji wa elimu ya mazingira utaleta mabadiliko makubwa katika mazingira na mabadiliko hayo yaanzie katika maeneo ya karibu na kituo. 

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mkuu wa Divisheni ya Utumishi na Utawala, Bi. Renalda Mbowe amesema mbali na Halmashauri ya Mji Masasi kuchangia viwanja viwili vyenye thamani ya Tsh milioni 20 katika Ujenzi wa hicho, Halmashauri itaendelea kuhakikisha ustawi wa kituo hicho unadumu na kuleta manufaa kwa jamii. 

Diwani Kata ya Napupa, Mhe. Sospeter Nachunga amesema ujenzi wa kituo hicho utaleta mapinduzi katika kujenga uelewa na kuzuia uchafuzi wa Mazingira na utenganishaji wa taka katika jamii ya Masasi. 

Kaimu Mkuu Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Bi. Anna Hokororo, amesema ujenzi wa Mradi wa Kituo cha Mazingira unaotekelezwa katika Mtaa wa Wapiwapi A kata ya Napupa unahusisha ujenzi wa ukumbi wa mafunzo, ofisi ya wataalamu wa Mazingira na Nishati, mgahawa, sehemu ya kupumzikia, jiko, vyoo, ujenzi wa uzio na kisima cha uvunaji wa maji ya mvua.

Amesema ili kulinda Mazingira, mradi huo umetumia chuma kwenye kupaua, milango na madirisha ili kupunguza matumizi ya mazao ya misitu ili kulinda Mazingira na kwamba Ujenzi wa kituo hicho umegharimu jumla ya Tsh milioni 242,763,254 zilizotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Enzkreis ya Ujerumani. 

Meneja wa Kituo hicho, Bi. Catherine Tendeje amesema kituo hicho kimelenga kutoa elimu ya mazingira na kuimarisha ustawi wa viumbe hai na uoto wa asili kwa kujenga uelewa na uanzishwaji wa vitalu vya miti, nishati mbadala mfano biogas na solar, uelewa na utengenezaji wa matumizi ya majiko sanifu.

Mratibu wa Ushirikiano kutoka Halmashauri ya Mji Masasi Ndg. Kajuti Nyambi amesema ushirikiano huo ulianza mwaka 2011 ambapo Halmashauri ya Mji na Wilaya zimekuwa zikinufaika katika nyanja mbalimbali zikiwemo afya, elimu, mazingira, nishati mbadala (ufungaji wa Umeme wa Jua) na michezo kwa kupata misaada mbalimbali ya kimaendeleo. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.