• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MAAFISA UGANI KANDA YA KUSINI WAPIGWA MSASA

Posted on: March 21st, 2024

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Machi 21, 2024 imeendelea na zoezi la kuwanoa maafisa ugani wa sekta ya Mifugo waliopo kanda ya kusini inayojumuisha mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye mafunzo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Jengo la Utawala, Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Lauter Kanoni amewasisitiza maafisa ugani hao kuhakikisha wanatumia mafunzo hayo kwenda kubadili mfumo wa ufugaji kutoka ule wa holela hadi ufugaji wa kisasa.

"Wakati wa msimu wa mvua hali ni shwari lakini ikifika kiangazi sisi na nyie Maafisa Mifugo huwa hatulali kila kukicha tunaenda kushughulikia migogoro baina ya wakulima na wafugaji hivyo tumieni mafunzo haya kuwabadili wafugaji waanze kufuga kisasa ili kuepusha madhara baina ya pande hizo mbili" Amesisitiza Mhe. Kanoni.

Aidha Mhe. Kanoni amewataka watalaam hao katika sekta ya Mifugo kutoa elimu kwa wafugaji juu ya umuhimu wa chanjo kwa mifugo ili kuepusha madhara kwa mifugo na watumiaji wa mazao ya Mifugo hiyo.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Maafisa Ugani wenzake, Daktari wa Mifugo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Bi. Subira Simbeye ameahidi kwenda kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Kanoni ili kuendelea kuboresha sekta ya Mifugo kwa mikoa ya Lindi na Mtwara.

Awali akiwasilisha mada ya "Sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia Utumishi wa Umma", Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Wizarani hapo Bi. Suzan Silayo amewataka Maafisa ugani hao Kufanya kazi kwa uadilifu, kuzingatia maadili ya utumishi na kufuata sheria kanuni na taratibu za kiutumishi.

"Pia mkafanye kazi bila upendeleo na muwe waaminifu wakati wote huku mkitoa ushauri kwa viongozi wenu pale inapobidi kwa kuwa wao nyie ndio wataalamu lakini wakati wote msisahau kutunza siri za serikali" Ameongeza Bi. Silayo

Aidha Bi. Silayo amewataka wataalam hao kuepuka kutoa au kupokea rushwa huku pia akiwasisitiza kujiandaa na maisha ya baada ya kustaafu katika Utumishi wa Umma kwa kuhakikisha wanafanya uwezekaji wa kutosha pindi wakiwa kazini.

Mafunzo hayo kwa Maafisa Ugani wa mikoa ya kanda ya Kusini yatafanyika kwa siku 2 ambapo mada mbalimbali zinatarajiwa kuwasilishwa kwa wataalam hao kwa lengo la kuwakumbuka taratibu mbalimbali za utekelezaji wa majukumu yao pindi wakiwa uwandani.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.