• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

ZIARA YA KAMATI YA FEDHA NA UTAWALA HALMASHAURI YA MJI MASASI.

Posted on: December 14th, 2022

Kamati  ya fedha na Utawala  halmashauri  ya Mji Masasi Mkoani Mtwara  imetoa agizo kwa wataalam wote ambao wanahusika kusimamia Miradi ya maendeleo kuhakikisha wanasimamia majukumu yao mpaka pale Mradi unapokamilika.

Ameyasema hayo  0ktoba 20,2022 Mwenyeketi wa kamati ya fedha na Utawala Mh: Hashim Namtumba  ambae pia ni diwani wa kata ya Jida katika ziara ya ukaguzi  wa miradi ya Maendeleo  katika robo ya kwanza kwa mwaka wa Fedha 2022/2023.

Katika ziara hiyo kamati imetembelea na kukagua Miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa sekondari mpya ya Temeke ,ujenzi wa Jengo la kujifungulia zahanati ya Chisegu,Ujenzi wa OPD na Maabara kituo cha Afya Mtandi ,Ujenzi wa choo Soko la Jida ,Ujenzi wa Vyumba vinne vya  Madarasa Shule ya Sekondari Anna Abdalla ,Ujenzi wa Zahanati ya Machombe .

Kupitia ziara hiyo kamati ya fedha ilipokea maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri Mji Masasi Elias Ntiruhungwa kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari ya Temeke amesema kuwa Halmashauri ilipokea fedha Shilingi 470,000,000.00 ambayo   haikutosha kutekeleza Mradi Wote kulingana na Mchoro wa BOQ ya Mradi hivyo hadi kukamilisha Ujenzi  wa Majengo yote yaliyoopo kwenye  Mchoro ilihitajika fedha Shilingi 700,000,000.00.

’Baada ya kuona fedha hazitoshi Halmashauri iliamua kuanza ujenzi  kwa kujenga Majengo ambayo yataweza kupokea wanafunzi na kufanikiwa kujenga jingo la utawala,Vumba 8 vya Madarasa ,Maabara ya kemia na biolojia ,vyoo vya wavulana na Wasichana ambavyo vimekamilika ,na Jengo la Maktaba ambalo bado halijakamilika na tunatarajia kupokea wanafunzi ifikapo januari 2023 kwa sababu shule hii tayar imeshasajiliwa’’Elias Ntiruhungwa.

Baada ya kupokea maelezo hayo kamati imepongeza menejimenti  kwa mawazo mazuri ambayo pamoja na Majango kutokamilika kulingana na Mchoro  kama  ulivokuwa unatakiwa  ukamilishwe ila ni hatua ambayo imeleta matumaini yakuweza kutumika  pale ifikapo January 2023.

Katika ziara hiyo kamati ya Fedha na Utawala imekagua ujenzo wa jengo la kujifungulia Zahanati ya Chisegu  ambapo Mtendaji  Kata Zakia Maguno  alisoma Taarifa ya Mradi na kueleza  vyanzo  vya  fedha  vya Mradi huo kuwa ni Mfuko wa Jimbo  ulitoa Shilingi 14,100,000 Nguvu za wananchi   Shilingi  500,000  Mfuko wa Afya Shilingi 3,795,000 pamoja na mapato ya Ndani ya halmashauri   Shilingi 1,000,000 na Jumla kuu  ni Shilingi 19,395,000  ambayo imeweza kukamilisha Mradi huo.

Kamati imepokea taarifa hiyo na kuridhia kwani Maendeleo ya Mradi ni  Mazuri yanaonekana na Thamani ya fedha iliyotumika ni sahihi pia wametoa Shukrani kwa halmashauri ya Mji Masasi kwa kuwawezesha kukamilika kwa Mradi huo ambao ni msaada mkubwa kwa wakazi wa kata hiyo.

Vilevile kamati ilifanya ziara katika ujenzi wa zahanati ya Machombe ambapo wajumbe walishuhudia juhudi zilizofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wananchi wa kata hiyo ambapo Mradi  huo utagharimu kiasi cha fedha  shilingi  106,776,692.00 mpaka kukamilika na hadi sasa Mradi umepokea Fedha shilingi  62,000,000 ikiwa mradi upo hatua  ya  uchapiaji.

Hivyo kamati imeridhishwa na mradi huo baada ya kukaguwa na wametoa pongezi kwa wasimamizi wa Mradi huo pia kamati imeshauri zifuatwe taratibu zote za manunuzi ili kuepuka hoja za kiukaguzi.

 pia wametoa agizo kwa Mhandisi wa halmashauri ya Mji Ombeni Usiri kuandaa BOQ kwa ajili ya ujenzi wa choo ambayo itatumika baada ya kunza kutoa huduma katika zahanati hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.