• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

“VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

Posted on: May 15th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara CPA. Bahati Geuzye ameziagiza Wilaya na Halmashauri zote za Mkoa wa Mtwara kuhakikisha vituo vyote vya kutolea huduma za afya  vinaweka kipaumbele  katika utoaji wa  huduma za Tiba Okovu na Huduma Msingi kwa Wagonjwa Mahututi (Essential Emergency and Critical Care) ambayo ni huduma nafuu na yenye ufanisi.

Amesema hayo Mei 15, 2025 wakati akifungua mafunzo ya watoa huduma za afya wapatao 144 yanayofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) yanayohusu  Tiba Okovu na Huduma Msingi kwa Wagonjwa Mahututi (Essential Emergency and Critical Care) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mwambe Royal Court Halmashauri ya Mji Masasi.

Aidha ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi kubwa za kuboresha huduma za afya kwa kutoa fedha nyingi katika Mkoa, Wilaya na Halmashauri za Mtwara hususani ujenzi wa miradi ya afya, ununuzi wa vifaa tiba, kuwezesha upatikanaji wa dawa kwa wingi na ajira mpya kwa watoa huduma za afya.

Akizungumza Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Peter Majura Esanju amesema mafunzo hayo yanalenga kuokoa Maisha ya wagonjwa mahututi katika ngazi zote za kutolea huduma za afya hususani ngazi za msingi ambazo ni zahanati, kituo cha afya na hospitali za Halmashauri yakihusisha watumishi 144 wanaopata mafunzo kwa awamu kutoka Manisipaa ya Mtwara Mikindani na Nanyumbu kwa kuanzia na hadi sasa waliopata mafunzo ni watumishi 82.

Naye, Mshauri wa Ufundi kutoka UNICEF, Frank Eetaama amesema shirika hilo limekuwa likishirikiana na Serikali katika mambo mengi katika sekta ya afya  ikiwemo huduma za mama na mtoto, uimarishaji wa mifumo na mafunzo mbalimbali yakiwemo ya  Tiba Okovu na Huduma Msingi kwa Wagonjwa Mahututi (Essential Emergency and Critical Care) na kuomba ushirikiano huo kuendelea ili kunufaisha wananchi kwa huduma mbalimbali.

Picha mbalimbali za Matukio katika mafunzo.






Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.