• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

VIONGOZI WAPONGEZA HALMASHAURI YA MJI MASASI KWA KUPATA HATI SAFI

Posted on: June 19th, 2023

Viongozi mbalimbali wa Serikali wameipongeza Halmashauri ya Mji Masasi kwa kupata hati safi (Unqualified Opinion) katika taarifa ya Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Akizungumza June 13, 2023 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la kupitia taarifa za Mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali, Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Ahmed Abbas Ahmed aliwapongeza viongozi wa Halmashauri hiyo kwa kazi kubwa ya usimamizi wa miradi mbalimbali ya serikali.

Alisema usimamizi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye ngazi ya halmashauri na kata ni jukumu la kila mmoja bila kuwaachia watu wachache.

“Lakini niwapongeze zaidi kwa kupata hati safi (Unqualified Opinion)… lakini pia Halmashauri ihakikishe miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yake inakamilika kwa wakati uliopangwa ili kuondokana na hoja zinazotokana na halmashauri kushindwa kukamilisha miradi kwa muda uliopangwa,” Mkuu wa Mkoa.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Lauter John Kanoni alisema hati safi ndio kipimo cha utendaji na kuwapongeza waheshimiwa madiwani kwa kusimamia utendaji wa halmashauri hiyo uliosababisha kupatikana kwa hati safi huku akiwataka watendaji kutekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.

“Nawapongeza Halmashauri ya Mji Masasi kwa kupata hati safi, na ndio kipimo, tungekuwa na hati isiyoridhisha hapa kila mtu uso wake usingekuwa na tabasamu, hii inadhihirisha kuwa waheshimiwa madiwani mnasimamia halmashauri vizuri” Mkuu wa Wilaya.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Masasi, Mhe. Mariam Kasembe aliwataka watendaji na menejimenti kuongeza juhudi ili mwaka ujao wa fedha halmashauri ipate hati safi nyingine.

“La mwisho, naomba nipongeze kwa kupata hati safi, naomba tukaze buti mwaka kesho msituangushe tupate hati safi tena,” Mwenyekiti wilaya CCM.

Akitoa taarifa ya mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali, Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Masasi, Bi. Erica Yegella alisema kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri hiyo ilikuwa na hoja sita huku hoja moja ikiwa imefungwa na tano zikiendelea.

“Halmashauri ya Mji imepokea taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali inayohusu mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni 2022, taarifa hii imelenga kuwajulisha matokeo ya ukaguzi na mapendekezo yaliyotolewa wakati wa ukaguzi, katika taarifa hiyo halmashauri ya Mji imepata hati safi,” Bi. Erica Yegella.

Awali, Kaimu Mkaguzi mkuu wa nje, Mkoa wa Mtwara, Bi. Mary Wembe alisema katika kipindi chote cha ukaguzi ofisi ya mkaguzi ilipata ushirikiano kutoka kwa wafanyakazi na menejimenti ya halmashauri ya mji Masasi.

“kwa niaba ya ofisi ya taifa ya ukaguzi ya hesabu za serikali napenda kuwapongeza halmashauri ya Mji Masasi kwa kupata hati safi,”-Mary Wembe.

Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano jengo la utawala, Halmashauri ya Mji Masasi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.