• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

UZINDUZI WA KAMPENI YA UHAMASISHAJI NA UTOAJI WA CHANJO ZA MIFUGO, SERIKALI YATOA RUKUKU, CHANJO YA KUKU BURE.

Posted on: January 8th, 2025

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi  Mhe. Hamisi Nikwanya kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri leo Januari 8, 2025 amezindua rasmi zoezi la kampeni ya uhamasishaji wa chanjo ya Mifugo  itakayotolewa kwa ruzuku na Serikali dhidi ya magonjwa matatu ya mifugo kwa Ng`ombe (Homa ya mapafu), Mbuzi, Kondoo (Sotoka) na Kuku (Kideri) ambapo uhamasishaji wa chanjo hiyo utafanyika  kwenye kata 14, vijiji 31 na Mitaa 57 ya Halmashauri ya Mji Masasi. 

Amesema uhamasishaji huo ni jitihada na juhudi kubwa zilizofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kutoa chanjo za mifugo kwa kutenga kiasi kikubwa cha fedha ambapo kwa mwaka huu wa fedha 2024/2025 jumla ya Tsh Bilioni 28.1 zimetolewa ili kufanikisha zoezi hilo. 

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Masasi Ndg. Andrea Kalinga amewataka watalaam waliojengewa uwezo  kuhusu zoezi la utoaji wa chanjo ambao ni maafisa mifugo, uvuvi na kilimo Kwenda kufanya kazi kwa kujitoa kwa dhati na uadilifu wa kiwango cha juu ili kuweza kuwasaidia wafugaji.

Akieleza kuhusu mpango huo Daktari wa Mifugo Halmashauri ya Mji Masasi Dkt. Vailet Mhehe amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeandaa mpango wa miaka mitano wa kutoa chanjo dhidi ya magonjwa matatu ya mifugo  kwa wakati mmoja Nchi nzima kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo ambayo ni Homa ya Mapafu ya Ng`ombe (CBPP), Sotoka kwa mbuzi na kondoo (PPR) na Kideri kwa Kuku.

Amesema katika mpango huo, wafugaji watachangia gharama ndogo sana ya utoaji wa  chanjo hizo ambapo  Ng`ombe ni Tsh 500, Mbuzi na Kondoo Tsh 300 na kwa Kuku chanjo itatolewa bure, kuanzia Januari 25, 2025. 

Ameongeza kuwa faida za utoaji wa chanjo hiyo ni pamoja na kupunguza vifo vya mifugo, kuwapunguzia wafugaji gharama za kununua chanjo wenyewe, kuongeza soko la mifugo ndani na njee ya Nchi, kutoa ajira za moja kwa moja na kuwezesha viwanda vinavyotumia mifugo au mazao ya mifugo. 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.