• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

Rais Magufuli azindua kituo cha Afya Mbonde Wilayani Masasi.

Posted on: April 5th, 2019

Rais  wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amefungua  kituo cha Afya  Mbonde  kilichopo Halmashauri ya Mji Masasi  mkoani Mtwara kikiwakilisha vituo 352 vilivyojengwa kote nchini kwa kipindi cha miezi 18 yaani tangu  mwezi Disemba 2017 hadi saa kupitia mpango wa maboresho ya  afya.

Mhe. Rais alifanya ufunguzi huo, akiwa kwenye ziara ya kikazi Mkoani Mtwara na kueleza kuwa kituo cha Afya Mbonde kilichogharimu shilingi milioni 500 ni kati ya vitu 13 vilivyojengwa Mkoani Mtwara vikiwa na uwezo wa kutoa huduma za matibabu mbalimbali ikiwemo upasuaji kwani ina vifaa vya kisasa.

Mhe. Rais ameeleza kuwa “nimekuja kufungua kituo hiki cha Mbonde kwa niaba ya vituo vyote 352 vinavyojengwa nchi nzima baada ya kujiridhisha hatua za ujenzi kwa kila kituo, nawapongeza sana Masasi kwa ujenzi mzuri ulioendana na thamani ya fedha”

Mhe. Rais amefafanua kuwa, Vituo hivi vimejengwa kwa fedha za serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo Benki ya Dunia, Kanada, Serikali ya Ujerumani, UNICEF na wengine, “ nawashukuru sana kwa mchango wao wa kuimarisha afya za wananchi”

Mhe. Rais ameeleza kuwa, Serikali imetumia jumla ya shilingi bilioni 184 kujenga vituo vyote 352 nchi nzima kwa lengo la kuboresha huduma za uhakika za matibabu katikakaribu na maeneo wanayoishi

Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amesema, Serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kujenga vituo vya Afya 352 na Hospitali 67 nchi nzima kwa muda wa miezi 18 ambapo kwa Mkoa wa Mtwara hospitali 3 zinajengwa katika wilaya za Mtwara, Masasi na Nanyamba ukilinganisha na hospitali 77 zilizokuwa zimejengwa tangu Uhuru.

Mhe. Jafo ameeleza kuwa “Ofisi ya Rais TAMISEMI inatekeleza ahadi za Rais kwa kusimamia miradi inayogusa wananchi wanyonge ikiwemo afya kupitia Mpango wa maboresho ya afya kwa katika ngazi za serikali za chini kabisa”

Kwa mujibu wa Mhe. Jafo, Ujenzi wa miradi hii ya afya unatumia mafundi wa kawaida, hivyo kwa miradi yote inayotekelezwa watanzania zaidi 7000 wamepata ajira mbalimbali na kujiongezea kipato.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.