• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

NENDENI MKASIKILIZE NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Posted on: September 17th, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka Viongozi wa ngazi zote kwenda kusikiliza na kutatua kero za wananchi na kuacha tabia ya kukaa maofisini.

Mhe. Rais Samia ametoa maagizo hayo Septemba 17, 2023 wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Boma uliopo Halmashauri ya Mji Masasi mkoani Mtwara .

Ameeleza kusikitishwa kuona kero za Wananchi wa Vijijini zinafika mpaka Ikulu wakati kwenye maeneo yao kuna Viongozi wa ngazi zote.

Mhe. Rais amesema,

 “Nitoe wito kwa Uongozi mzima wa Mkoa na ngazi zote hadi Uongozi wa Vijiji na Mtaa kusikiliza na kutatua kero za Wananchi, Waziri wa TAMISEMI amelisema vizuri hapa nami naomba nimuunge mkono, mtakaposhuka jamani, nyinyi sio Watawala, hata Mimi sio Mtawala, Mimi ni Mtumishi wa Wananchi, Mawaziri wangu ni Watumishi wa Wananchi, tuliowashusha chini huku kutuwakilisha ni Watumishi wa Wananchi”

“Unapoacha kiti cha Utumishi ukakaa kiti cha Utawala ndio maana huwezi kushuka kwa Mwananchi kwenda kumsikiliza, niombe sana Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) simamieni hilo, Serikali hii mmeiweka nyinyi sasa mkijifanya wadogo na kufanya Watendaji kuwa wakubwa mnakosea, wasimamieni Watendaji warudi wakasimamie Wananchi”

Amesema haivumiliki kero za wananchi kufika ngazi za juu wakati kuna viongozi katika kila ngazi.

“Haipendezi kuna wasimamizi wa shughuli za Wananchi ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata mpaka Vijiji lakini unapokea pale Ikulu kero ya Mwananchi wa Kijiji inakuja kule Ikulu, haipendezi, tuliowaweka kwenye ngazi hizo mna kazi gani!?, kaeni vizuri fanyeni kazi zenu vinginevyo hatutowavumilia kupokea tena kero za Wananchi kule Ikulu wakati huku kuna Viongozi wapo”

Mhe. Rais Samia amehitimisha ziara yake aliyoifanya katika mkoa wa mtwara kuanzia Septemba 14, hadi Septemba 17, 2023 ambapo amezindua miradi mbalimbali muhimu ikiwemo ya afya, maji, barabara na kuzungumza na wananchi katika maeneo yote.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.