• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MKUU WA MKOA WA MTWARA MHESHIMIWA GELASIUS GASPAR BYAKANWA AIPONGEZA HALMASHAURI YA MJI MASASI KWA KUPATA HATI SAFI YA UKAGUZI KWA MWAKA 2018/2019

Posted on: June 4th, 2020

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano –Masasi Mji

Halmashauri ya Mji Masasi imepata pongezi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Gaspar Byakanwa kutokana na kupata hati safi ya ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha ambao umeishia mwezi Juni 2019.

Mheshimiwa Byakanwa alitoa pongezi hizo leo kwenye kikao maalum cha Baraza la Madiwani kilichoketi kwa ajili ya kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG); Kikao ambacho kilifanyika katika ukumbi wa Saint Jordan Migongo Mission.

Mheshimiwa Selemani Mzee, Mkuu wa Wilaya ya Masasi akimkaribisha Mkuu wa Mkoa ili aweze kuongea na Wajumbe wa Mkutano.

Katika ukaguzi huo wa hesabu za serikali kuanzia Julai mosi 2018 hadi mwezi Juni 2019, Halmashauri ya Mji Masasi ilikuwa na jumla ya hoja 20, ambapo kati ya hoja hizo, hoja 9 zilipatiwa majibu na kufungwa, wakati hoja 1 ilihamishiwa mamlaka ya maji vijijini (RUWASA), na hoja 10 zinaendelea kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Hamisi Ausi Mnela (Kisiki cha Mgomba), Diwani wa Kata ya Matawale, akichangia hoja wakati wa kuijadili taarifa ya CAG.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, mbali na pongezi hizo ameiagiza menejimenti ya Halmashauri ya Mji Masasi ihakikishe inaongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato na kubuni vyanzo mbalimbali vya mapato ambavyo vinatekelezeka ndani ya muda mfupi.

Mheshimiwa Byakanwa, alitumia nafasi hiyo pia, kutoa elimu juu ya virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19 kwamba ijapokuwa maambukizi ya ugonjwa huo yamepungua kwa kiasi kikubwa, bado wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari zinazoelekezwa na wataalamu wa afya ikiwa ni pamoja na kufanya mazoezi kwa lengo la kumarisha kinga ya mwili.

Akifunga Mkutano huo maalum, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi Mheshimiwa Sospeter Nachunga, alitoa shukrani zake za dhati kwa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na msafara wake kwa ujumla kutokana na maelekezo na miongozo mizuri ambayo ameitoa kwenye mkutano huo, kwa kuwa yote yamelenga katika kuboresha ufanisi na kuinua maendeleo ya Halmashauri ya Mji Masasi.

Mheshimiwa Sospeter Nachunga, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi akimshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kabla ya kufunga Mkutano

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.