• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

Mkuu wa Mkoa Mtwara aendelea na Kampeni ya Shule ni Choo Wilayani Masasi

Posted on: September 21st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Gaspar Byakanwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Masasi na Halmashauri ya Wilaya Masasi (hawapo pichani)

Na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Masasi Mji

“Tunapaswa kuondokana na upungufu wa vyoo, nimeamua kulibeba jukumu hili baada ya kugundua choo ni tatizo kwenye Shule zetu”, Kauli hiyo imetolewa Jumamosi tarehe 21/09/2019 na Mheshimiwa Gelasius Gaspar Byakanwa, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara alipokuwa akizungumza kwenye kikao kilichohusisha Wakuu wa Idara na vitengo, Waheshimiwa Madiwani, na Wakuu wa Taasisi mbalimbali zilizopo Wilayani Masasi.

katika kikao hicho Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa aliwahamasisha Wajumbe na wananchi wa Wilaya ya Masasi kwa ujumla kuchangia ujenzi wa vyoo bora vya Wanafunzi na Walimu kwenye Shule za Msingi na Sekondari ili kuyafanya mazingira ya kufundishia na kujifunzia kuwa rafiki kwa Walimu na Wanafunzi.

Akitoa takwimu za mahitaji ya matundu ya vyoo kwenye Shule zilizopo Mkoani Mtwara, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa alisema, Matundu ya vyoo ambayo yanahitajika ni 6547 kwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari, wakati matundu 1830 yanahitajika kwa ajili ya Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari.

Kupitia harambee aliyoiendesha kwenye kikao hicho cha Watumishi, huku akisisitiza ya kwamba jukumu la ujenzi wa vyoo kwenye shule zilizopo Mkoani Mtwara ni la wana Mtwara wote, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa alifanikiwa kupata ahadi ya kiasi cha Tsh.8,210,000/=, Saruji mifuko 27, na matundu manne ya vyoo ambapo hadi kufikia tarehe 10/10/2019 ahadi zitakuwa zimekamilishwa.

Aidha, Mheshimiwa Byakanwa aliwataka watumishi kushiriki vyema kwenye maandalizi na uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 24/11/2019, “Kuanzia tarehe 8/10/2019 hadi tarehe 14/10/2019 Kutakuwa na zoezi la kuandikisha wapiga kura ambao ni wakazi wa eneo husika, Wananchi wenye sifa wahamasishwe kujiandikisha na kugombea nafasi mbalimbali.” Alisisitiza Mheshimiwa Byakanwa.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, alitumia kikao hicho kuwafunda Watumishi na Madiwani wa Halmashauri zote mbili kuona umuhimu katika suala zima la kuwekeza. Alisema kutowekeza kunasababisha kupungua kwa wigo wa ajira kwa sababu wenye fursa ya kuwekeza hawafanyi hivyo.

Mheshimiwa Byakanwa, akiwa Wilayani Masasi jana Jumamosi amefanya vikao vitatu tofauti kwa lengo la kuhamasisha Wadau na wananchi Wilayani humo kuchangia ujenzi wa vyoo vya Walimu na Wanafunzi chini ya Kampeni aliyoiasisi ya “SHULE NI CHOO.” Pamoja na Kuhamasisha ushiriki wa Wananchi kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, chini ya kauli mbiu isemayo “Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa ni Chachu ya Mendeleo, ni Haki na Wajibu Wako Kujiandikisha, Kugombea, na Kuchagua Kiongozi Bora.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.