• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Awaagiza Viongozi Kuwakemea Watakaonza Kampeni za Uchaguzi Mkuu Kabla ya Muda

Posted on: January 13th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mheshimiwa Selemani Mzee  amewaagiza viongozi wa ngazi mbalimbali Wilayani humo kuwakemea watu wote ambao watajitokeza kwa wananchi na kuanza kufanya kampeni kabla ya muda.

Mheshimiwa Selemani Mzee amesema kufanya kampeni kabla ya vikao rasmi ndani ya chama husika kufanyika ni kusababisha vurugu kwa wananchi. Alisisitiza ya kwamba Wilaya ya Masasi haipo tayari kuruhusu vurugu ambazo zitasimamisha shughuli za maendeleo.

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa agizo hilo leo baada ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kwenye Ofisi ya Mtaa wa Wapiwapi A, Kata ya Napupa, Halmashauri ya Mji Masasi.

Akizungumzia zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, Mheshimiwa Selemani Mzee amewataka Wananchi wa Wilaya ya Masasi ambao wana umri wa miaka 18 na kuendelea na wale ambao watatimiza umri wa miaka 18 siku ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kujitokeza kwa wingi ili waweze kujiandikisha na kupata vitambulisho vitakavyowawezesha kupiga kura.

Alisisitiza ya kwamba zoezi hilo pia ni fursa kwa kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama kutoka Kata moja kwenda nyingine, Jimbo moja kwenda jingine n.k. Lakini pia kwa waliopoteza vitambulisho vyao au kuharibika, ni wakati muafaka kwao kupata vitambulisho vipya.

Zoezi la Kujiandikisha/kuboresha daftari la wapiga kura kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara limeanza jana Jumapili tarehe 12/01/2020 na litakamilika Jumamosi ya tarehe 18/01/2020.

Kwa mujibu wa Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Masasi Mjini Ndugu Gresha Sanga, jana ambayo ni siku ya kwanza ya zoezi hilo jumla ya watu 2961 wamejiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, wakati watu 1667 wameboresha taarifa zao na kupatiwa vitambulisho vipya baada ya kubadilisha makazi yao, na watu 12 wamefutiwa taarifa zao kutokana na kukosa sifa ikiwa ni pamoja na kufariki. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.