• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KUSINI 2018 YAFUNGULIWA, VIJANA WAELIMISHWE KUWEKEZA KATIKA KILIMO ,MIFUGO NA UVUVI

Posted on: August 5th, 2018

Ili viwanda viweze kuendelea katika uzalishaji wa bidhaa mbalilimbali na kuifanya nchi kufikia uchumi wa kati, vijana lazima wapewe elimu zaidi ya namna ya kutumia fursa ya kuwekeza katika kilimo. Mifugo na Uvuvi ili kuwezesha uzalishaji mkubwa wa malighafi ambazo zitatumika katika viwanda hivyo huku wao wakijiongezea uchumi

Msisitizo huo ulitolewa juzi na mgeni rasmi mhe Shaib Ndemanga rasmi wakati wa kufungua maonesho ya Nanenane kanda ya kusinikwa mwaka 2018 yanayofanyika katika viwanja vya Ngongo Manispaa ya lindi na kueleza kuwa vijana ndio nguvu kazi ya Taifa hivyo ni vema wakaelimishwa na kuwezeshwa kutambua fursa hiyo adhimu ya kuwekeza katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kama fursa ya kukuza uchumi wa nchi.

Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe Selemani Mzee akisalimia Wananchi Waliohudhuria Sherehe za Ufunguzi wa Nanenane katika Viwanja Vya Nanenane Manispaa ya Lindi.

Mheshimiwa Ndemanga ameeleza kuwa maonesho ya nanenane kwa mwaka 2018 yameendelea kuonesha teknologia mbalimbali za kilimo mifugo na uvuvi, hivyo ni fursa nzuri kwa wananchi wote wa kanda ya kusini kwenda kujifunza njia za kisasa za uzalishaji wa mazao ya kilimo mifugo na uvuvi na hatimaye kuongeza uchumi katika jamii na taifa kwa ujumla.

“Tuanaamini, kama watu watalima, watafuga na kuvua kibiashara watazalisha ajira nyingi kwa wananchi wakiwemo vijana na hivyo kupunguza tatizo kubwa la ajira lililopo sasa, tumieni maonesho haya kama shamba darasa kujifunza teknologia mbalimbali ili muweze kuzalisha kwa tija” alisema Ndemanga

Ndemanga alifafanua kuwa zaidi ya 70% ya watanzania wanategemea sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi hivyo ni lazima sekta hizi ziboreshwe ili watanzania waweze kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda ambalo ndilo lengo la serikali.

Kauli mbiu ya maonesho ya Nanenane 2018 inasema “wekeza katika kilimo,mifugo na uvuvi kwa maendeleo ya viwanda” hivyo ni wajibu wa kila mtu kutambua fursa kwa kuwekeza ili kuzalisha malighafi za kutosha kwa ajili ya kuendeleza viwanda vya ndani na hatimaye kuisaidia serikali kupunguza gharama za kuagiza vitu kutoka nje ya nchi.

Aidha serikali imeendelea kufuta na kupunguza ada na tozo ikiwemo tozo 80 kati ya 139 za kilimo zimefutwa, kwenye ushirika tozo 20 zimefutwa na katika sekta ya mifugo tozo 7 zimefutwa ambazo zilikuwa kero kwa wakulima, wafugaji na wavuvi lengo ikiwa ni kuwapunguzia wakulima tozo na ada zisizo za lazima.



Moja ya Vitalu vilivyopo kwenye Banda la Halmashauri ya Mji masasi


Maonesho ya Nanenane kwa kanda ya kusini inashirikisha halmashauri 15 za mikoa ya lindi na Mtwara pamoja na taasisi zingine za serikali na binafsi, maonesho haya kwa kanda ya kusini yalianza rasmi kufanyika mwaka 2004.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.