• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

MAKALA: ZIARA YA DKT SAMIA "YAIFUNGUA" MASASI MJI NA KULETA "NURU" KWA WANANCHI

Posted on: September 19th, 2023

Ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Halmashauri ya Mji Masasi Masasi "Imeifungua" Masasi  Mji na kuleta "Nuru" kwa watoto, wakina mama, vijana, wazee, wakulima, wafugaji, wagonjwa na wananchi wote wa Masasi.

Shamrashamra zilianza mapema Septemba 9, 2023 mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Ahmed Abbas Ahmed kutangaza ziara ya  Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba Septemba 14 hadi Septemba 17, 2023 mchana na usiku atahamia mkoani humo.

Ilikuwa ni habari mpya, kubwa na yenye msisimuko kwa wananchi wa Mtwara. Hatimaye Septemba 14, 2023 Mhe. Rais Samia aliwasili rasmi Mtwara na kupokelewa na maelfu ya wananchi wa mkoa huo.

Ujio huo ulizidi kuenea na kusambaa kwa kasi baada ya ratiba ya Mhe. Rais Samia kuonesha atatembelea Masasi Mji. 

Maarufu kama "Kariakoo" ya Mtwara kama alivyobainisha Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Lauter John Kanoni wakati akiwatambulisha viongozi akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi, Mhe. Hashim Namtumba sambamba na Mkurugenzi wa Mji Masasi Bi. Erica Yegella kwa maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa Rais Dkt Samia uliofanyika katika uwanja wa boma Masasi mjini Septemba 17, 2023.

"Mji huu wa Masasi ni mji wa kibiashara, hapa ni katikati ya maeneo yote, halmashauri zote zinakuja kutafuta mahitaji yao hapa, kariakoo yao ni hapa" anasema Mhe Kanoni.

Mji huu upo kilomita 210 kusini magharibi mwa mkoa wa Mtwara, ukiwa na ukubwa wa hekta 37,920  huku idadi ya watu kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi 2022 ikiwa ni watu 137,585 wanaume wakiwa 65,781 na wanawake 71,804 wakiupamba Mji kwa shughuli za kilimo cha Korosho, ufuta, mbaazi na mazao mbalimbali ya chakula.

Mji huu unafikika kwa urahisi kutoka pande zote za nchi kwani ni makutano makuu ya barabara kuu ya Tunduru-Songea- Lindi-Dar es salaam-Mbeya, Nachingwea-Liwale-Newala- Tandahimba ukipambwa na hoteli za kifahari, masoko ya bidhaa, viwanda na viwanja vya uwekezaji.

Lakini pia, mtandao wa barabara umeimarishwa kama anavyobainisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa  kuwa mtandao wa barabara unaongezwa kutoka kilometa 6.9 hadi kilometa 11.2.

" Wana masasi wanakushukuru sana Mhe. Rais kwa kazi hii ya kuongeza mtandao wa barabara na kuongeza taa za barabarani" anasema Mhe. Mchengerwa.

Lakini pia, Nuru kwenye sekta ya afya imepatikana kama alivyobainisha Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini, Mhe. Geoffrey Mwambe wakati akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Masasi.

"Mhe.Rais nakushukuru sana kwa kung'arisha Masasi, Mji unang'aa Mji ni mpya  barabara za lami ziko nyingi na zinapendeza na upande wa afya zaidi ya shilingi bilioni 2 umetuletea wanamasasi kwa ajili ya ukarabati wa hospitali yetu  ya wilaya Mkomaindo hadi kufikia 2025 hospitali yetu itakuwa mpya"

Aidha, Nuru ikapatikana kwenye sekta ya maji ambapo Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso amesema Serikali itatoa fedha kiasi cha Tsh milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa chanzo cha maji Nangowo ili maji safi ya uhakika na kutosha yapatikane Masasi na maeneo ya pembezoni.

Hatimaye, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan akahutubia maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano huo.

"Nawashukuru sana wananchi wa Masasi kwa kujitokeza kwa wingi namna hii, nashukuru kwa heshima mliyonipa"

Ujio wake katika Halmashauri ya Mji Masasi Masasi "Umeifungua" Masasi  Mji na kuleta "Nuru" kwa watoto, wakina mama, vijana, wazee, wakulima, wafugaji, wagonjwa na wananchi wote wa Masasi.

Nuru kwenye "Umeme" Mhe.Rais Samia amesema safari ya kuondoa adha ya kukatika kwa umeme ndani ya Masasi imeanza na Serikali imejizatiti katika hilo.

" Kwa sasa mkandarasi yupo kazini kuinganisha Masasi kwenye Gridi ya Taifa kutokea Ruvuma. Pia kuna mkandarasi anatoa umeme Ruangwa kupitia Nangugwa, ambao utakuwa tayari ifikapo Desemba mwaka huu. Baada ya miezi 18 umeme wa uhakika utakuwa umefika".

Nuru kwenye "Kilimo" mfumo wa stakabadhi ghalani umeleta mafanikio kwenye zao la mbaazi, wananchi wamepata ongezeko la thamani ya zao hilo lakini pia kuhusu korosho Mhe. Rais amesema Serikali inajenga kongani ya viwanda ili kuongeza thamani ya zao hilo.

"Suluhisho la kupata bei nzuri ya korosho ni kuongeza thamani korosho zetu. Katika kuongeza thamani tunajenga kongani ya viwanda, Maranje ambapo patakuwa na kituo cha kukoboa korosho zote za Mtwara. Korosho zitaongezwa thamani, ili tuuze korosho zilizotengenezwa.Tukiongeza thamani bei itakuwa nzuri".

Aidha akawakumbusha wananchi wa Masasi kutumia fedha kwenye mambo yenye tija sambamba na kusisitiza  suala la elimu kwa kupunguza tamaduni zinazochochea ongezeko la mimba utotoni.

 "Wachezeni wakiwa na umri mkubwa huku wakijua mambo wanayofundishwa" Mhe. Rais Dkt. Samia

Kazi iendelee " Nataka niwaambie ndugu zangu wa Masasi kwamba, Maendeleo yanakuja kwa vitendo na kwakuchukua hatua mahususi  na si kwa maneno. Maendeleo ni vitendo. Ninatoa rai kwa watanzania wote popote walipo kuunga mkono jitihada hizi za Serikali na kufanya kazi kwa bidii. Kama ni mkulima anza sasa kuongeza mashamba, ili mazao yawe mengi zaidi, kwani Serikali imejitoa kukuza kilimo kwa kiasi kikubwa", 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihitimisha ziara yake Mkoani Mtwara katika viwanja vya Boma, Halmashauri ya Mji Masasi.

Karibu Halmashauri ya Mji Masasi, Viwanja vya Biashara, Makazi na Uwekezaji vinapatikana, Karibu uwekeze Masasi.

Imetolewa na,

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.

Halmashauri ya Mji Masasi.

Septemba 19, 2023.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.