• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

Mafunzo wa Utengenezaji wa Tovuti kwa Maafisa TEHAMA na Maafisa Habari.

Posted on: March 21st, 2017

Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda amewaagiza na Kuwataka Maafisa Tehama na Maafisa Habari kufanya kazi kwa kuzingatia Miiko na Maadili ya Taaluma yanayoelekeza utoaji wa taarifa na matukio ya shughuli na miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo yao ili kuhabarisha umma kupitia taarifa sahihi.     

Katibu Tawala Luanda,ameeleza hayo wakati akifungua Mafunzo ya Uanzishaji na Uendeshaji wa Tovuti kwa Maafisa Tehama na Maafisa Mawasiliano wa ngazi za Mamlaka za Serikali za Mitaa za Mikoa,Halmashauri za Manispaa,Miji na Wilaya kwa taasisi hizo za Mikoa ya Kisini ya Mtwara,Ruvuma na Lindi yatakayofanyika kwa Wiki nzima kuanzia Leo,katika Ukumbi wa Mikutano wa Tiffany Diamond Hotel Mjini Mtwara.   

Luanda,amesema ni vyema Maafisa Habari na Tehama kuzingatia Maadili na Miiko ya Taaluma ya Habari katika masuala ya utoaji wa taarifa zilizo sahihi na zilizochungwa kutoka katika Mamlaka husika na chanzo cha kuaminika kwa lengo la kuwatarifu wananchi kuhusu Shughuli na Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayofanyika pamoja na matukio yoyote yanayofanyika katika Halmashauri zao na kuyatangaza kupitia Tovuti na Mitandao mbalimbali ya Kijamii na Vyombo vya Habari.

Amewaeleza na kuwasihi kujituma na kuwa Wabunifu katika utoaji wa Habari kupitia taarifa na matukio mbalimbali kwa kutumia kikamilifu vitendea kazi vilivyopo,"naomba mjitahidi sana kutoa taarifa kwa nyakati hizi za ukuaji wa Teknolojia hususan matumizi ya simu za Viganjani ama Mkononi ambazo zina uwezo wa kupiga picha nzuri za Mnato na Video zenye ubora na kuzirusha katika mitandao ya jamii"

.Alifafanua na kisisitiza Alfred Luanda.Awali akitoa Maelezo ya Utangulizi kuhusiana na Zoezi zima la Mafunzo ya Tovuti kwa Maafisa Habari na Maafisa Tehama,Kiongozi wa Mafunzo haya kwa Mikoa ya Kanda ya Kusini,Edgar Mdemu ambaye na Afisa Tehama wa Mkoa wa Simiyu alisema Mafunzo ni muhimu sana kwa Maafisa Tehama na Habari ili kuziwezesha Tovuti zote za taasis husika kufanya kazi na kuwa na taarifa za kutosha ikiwemo taarifa na habari mpya za kila siku.

Alifafanua na kueleza kuhusu lengo la Serikali kuimarisha na  kuboresha mifumo ya mawasiliano ya sekta za Umma kupitia ufadhili wa mradi wa Wamarekani USAID Ps3 kwa kwa ushirikiano na Tanzania,kwa uratibu na usimamizi wa Wakala wa Serikali Mtandao na Tamisemi,kwa lengo na madhumuni makubwa ya kuhakikisha kila taasis katika Mamlaka za Serikali za Mitaa inakuwa na Tovuti iliyohai.


Mdemu alieleza pia kwamba Mafunzo haya yanatolewa katika mgawanyo wa Kanda tank ( 5) Mikoa Kanda ya kati ya Dodoma ,Mikoa ya Kanda ya Morogoro,Mbeya na Kanda ya Kigoma,ambapo Mikoa ya Kanda ya Ziwa ya Simiyu,Mwanza,Mara,Kagera na Shinyanga zimeshafanya Mafunzo haya kwa Maafisa Tehama na Habari na Tovuti za Halmashauri na Mikoa hiyo zimekwishazinduliwa na zinafanyanya kazi kikamilifu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • “VITUO VYOTE VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MTWARA TUWEKE KIPAUMBELE CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA TIBA OKOVU NA HUDUMA MSINGI KWA WAGONJWA MAHUTUTI” RAS MTWARA.

    May 15, 2025
  • “WANANCHI TUJITOKEZE MKOMAINDO HOSPITALI KUPATA VIPIMO NA MATIBABU YA SARATANI BURE, SERIKALI IMELIPIA GHARAMA (SAMIA SULUHU OUTREACH SERVICES)” DC KASSANDA

    April 23, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA MASASI MJI, ZAIDI YA MILIONI 545 ZATOLEWA MWAKA HUU WA FEDHA 204/2025 KWA VIKUNDI 105 MIKOPO YA ASILIMIA 10.

    April 07, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA MASASI MJI WATOA ELIMU KUHUSU TAHADHARI YA UGONJWA WA MPOX

    April 06, 2025
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.