• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe za Watumishi |
Masasi Town Council
Masasi Town Council

Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Ofisa Ya Rais Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Mji Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara/Vitengo
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Mipango miji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Fedha
    • Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Biashara
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Utawala na Utumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Mipango miji na mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI LIMEPITISHA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 24 HALMASHAURI YA MJI MASASI.

Posted on: January 21st, 2023

 Baraza la  Madiwani Halmashauri ya Mji Masasi  limepitisha bajeti  ya shilingi 24,015,608,000.00    kwa ajili ya matumizi ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha ujao 2023/2024, Bajeti hiyo imejadiliwa na kupitishwa na Waheshimiwa Madiwani katika Mkutano Maalum wa Baraza la Halmashauri ya Mji Masasi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Masasi Mhe. Hashimu Hashimu Namtumba Kweka, ameliongoza Baraza hilo kwa kuwapitisha Waheshimwa Madiwani kujadili Mapendekezo ya Makisio ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024.

Waheshimiwa Madiwani wameipitia Mpango na Bajeti hiyo kipengele kwa kipengele na kisha kuipitisha kwaajili ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri kwa mwaka wa fedha ujao 2023/2024.

Mwenyekiti Halmashauri ya Mji Masasi Mhe. Namtumba amesema anaamini bajeti hiyo ambayo imepitishwa kwaajili ya utekelezaji wake kwa mwaka ujao wa fedha, itakidhi matakwa ya Halmashauri kwakuwa imekuwa bajeti iliyoelekezwa zaidi kwenye vipaumbele vya Halmashauri. “Tuna imani kubwa na bajeti hii kwa maana imeandaliwa vyema tofauti , hivyo ikitekelezwa katika uhalisia wake tutafikia malengo ya vipaumbele tulivyojiwekea”, aliongeza Namtumba.

Mkurugenzi  Halmashauri ya Mji Masasi, Elias Ntiruhungwa amesema kuwa utekelezaji wa bajeti unategemea na upatikanaji wa fedha, na anamini bila shaka bajeti iliyopitishwa na baraza la madiwani itasimamiwa vyema ili kutekeleza yale yote yaliyopendekezwa. “Tutasimamia vyema utekelezaji wa bajeti iliyopitisha, ili kuhakikisha vipaumbele vilivyobainishwa ikiwemo miradi ya maendeleo inatekelezwa”, alisema Ntiruhungwa.

Aidha, Ntiruhungwa amesema kuwa miradi mbalimbali na vipaumbele vilivyobainishwa itatekelezwa kwa wakati kwa kusimamia vyema mapato ya ndani ili kutekeleza miradi mbalimbali inayotokana na fedha za mapato ya ndani. “Tutaimarisha vikosi kazi, na mbinu mpya zitakazoongeza mapato ya Halmashauri kwa kiasi kikubwa ili kuwezesha utekelezaji wa bajeti hii”,  Ntiruhungwa .

Madiwani wamesema kuwa bajeti hii ina maono mazuri kwani imeainisha maeneo muhimu ambayo yataleta chachu kubwa ya Maendeleo ya Halmashauri ya Mji Masasi, Miongoni mwa vipaumbele vilivyobainishwa ni pamoja na utengenezaji wa miundombinu katika taasisi zikiwemo shule, Zahanati na vituo vya afya, Maeneo mengine ni pamoja ya kuimarisha ustawi wa jamii kwa kutoa Mikopo ya asilimia 10 ya Mapato ya ndani kwa Vijana ,Wanawake na walemavu.

Bajeti ya Halmashauri ya Mji Masasi  kwa mwaka wa fedha 2023/2024  imekisia kukusanya na kupokea  jumla ya  Shilingi  24,015,608,000.00  kati ya fedha hizo Mapato ya Ndani ni Shilingi 2,855,980,500.00 Ruzuku na Matumizi ya kawaida na Mishahara ni Shilingi 15,737,987,000  na Miradi  ya Maendeleo ni Shilingi 8,277,621,400.00 .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 28, 2020
  • TANGAZO LA KAZI April 05, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • TANGAZO LA KAZI May 23, 2022
  • Kuona Vyote

Habari Mpya

  • TUSHIRIKIANE KUTOKOMEZA VITENDO VYA UKATILI DC MASASI

    March 08, 2023
  • ZINGATIENI MATUMIZI YA POS

    January 21, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LIMEPITISHA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 24 HALMASHAURI YA MJI MASASI.

    January 21, 2023
  • KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI HALMASHAURI YA MJI MASASI (DCC)

    January 20, 2023
  • Kuona Vyote

Video

SHERIA ZA MITANDAO
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Sheria ndogo ya Ada na Ushuru kwa Mji wa Masasi

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Mtwara
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Rais UTUMISHI
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • SALARY SLIPS PORTAL

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MASASI TOWN COUNCIL

    Anuani ya Posta: P.O BOX 447 MASASI

    Simu Ya Mezani: +255 23 2510685

    Simu ya Kiganjani:

    Barua pepe: info@masasitc.go.tz

Mawasiliano

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@ Halmashauri ya Mji Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa.